Sidebar with Floating Button
MHUBIRI
AckyShine

Sala za kuheshimu Damu Takatifu ya Yesu

Featured Image

Tusali kila siku sala hizi, angalau kwa mwezi wa saba (Julai) kila mwaka, mwezi wa kuheshimu Damu Takatifu ya Mkombozi wetu.

Yesu alimwahidi Mt. Brigita wa Sweden kwamba wale watakaosali Baba Yetu 7 na Salamu Maria 7 kwa miaka 12 kwa kuheshimu damu yake takatifu na kutafakari juu ya Kutahiriwa kwake, jasho lake la damu, kupigwa kwake mijeledi, kuvikwa taji la miiba, kuchukua kwake Msalaba, kusuliwa kwake na kuchomwa ubavuni; watapata neema 5 zifuatazo: (1) Hawataingia toharani, (2) Yesu atawapa cheo cha mashahidi waliomwaga damu yao kwa ajili ya imani, (3) Yesu atawadumisha jamaa zake watatu katika hali ya neema, (4) Roho za jamaa zake zitakingwa na Jehanam mpaka kizazi cha nne, (5) Mwezi kabla ya kufa, Yesu atawajulisha. Wakifa kabla ya kutimiza miaka ile, watahesabiwa wamemaliza.

Ee Yesu, sasa ninataka kusali Baba yetu mara saba nikiungana na ule upendo ambao kwao uliitakasa sala hii katika Moyo wako. Uichukue kutoka mdomoni mwangu hadi moyoni mwako. Uiboreshe na kuikamilisha hivyo kwamba iupatie heshima na furaha kwa Utatu Mtakatifu kama vile Wewe ulivyoupatia kupitia sala hii wakati ulipokuwa bado hapa duniani. Utukuzwe ee Yesu, itukuzwe Damu Yako Takatifu sana uliyoimwaga kutoka katika Majeraha Yako Matakatifu.

1. Yesu anatahiriwa.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea Majeraha ya kwanza, maumivu ya kwanza na Damu ya kwanza aliyomwaga Mwanao mpenzi, Bwana wetu Yesu Kristu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu na dhambi za dunia nzima, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi ya kwanza ya mauti, hasa kati ya ndugu zangu.

2. Yesu anatokwa Jasho la Damu bustanini Gethsemane.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea mateso na mahangaiko makali sana ya moyoni, ya Bwana wetu Yesu Kristu katika mlima wa mizeituni na kila tone la jasho lake la damu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za kimoyomoyo, na dhambi za namna hiyo zinazotendwa na dunia nzima, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za moyoni na kwa ajili ya kueneza upendo wa kiMungu na wa kindugu.

3. Yesu anapigwa mijeledi.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea majeraha elfu elfu aliyopata, maumivu makali sana na Damu Takatifu sana aliyomwaga, alipopigwa mijeledi, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za tamaa ya mwili, kwa malipizi ya dhambi za tamaa ya mwili za wanadamu wote, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za tamaa ya mwili, na kwa kulinda usafi wa moyo, hasa kati ya ndugu zangu.

4. Yesu anavikwa taji la miiba.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea majeraha, maumivu na Damu Takatifu kutoka katika Kichwa Kitakatifu cha Yesu wakati alipovikwa taji la miiba, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za rohoni, kwa malipizi ya dhambi za rohoni za wanadamu wote, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za rohoni, na kwa ajili ya kueneza Ufalme wa Kristu hapa duniani.

5. Yesu anachukua Msalaba.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea mateso ya njia ya Msalaba, hasa donda lake la begani na Damu Takatifu iliyomwagika, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za ukaidi dhidi ya msalaba, na dhambi za ukaidi dhidi ya msalaba za wanadamu wote, malalamiko yote dhidi ya mipango yako mitakatifu na dhambi zote za ulimi, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za ulimi na kwa ajili ya upendo wa kweli kwa Msalaba.

6. Yesu anasulibiwa.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea Mwanao Msalabani, kupigwa kwake misumari na kuinuliwa kwake, madonda yake mikononi na miguuni na mifereji mitatu ya Damu yake Takatifu iliyomwagika kutoka katika majeraha haya, mateso yake makali sana ya mwili na roho, kifo chake kitakatifu, ukumbusho usio wa kumwaga wa damu wa kifo hiki katika Misa zote Takatifu ulimwenguni, kwa ajili ya majeraha yote yanayosababishwa na ukaidi wa nadhiri na kanuni katika madaraja matakatifu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu zote na za ulimwenguni mzima, kwa ajili ya wagonjwa na wanaokufa, kwa ajili ya mapadre watakatifu na walei, kwa ajili ya nia za Baba Mtakatifu za kukarabati familia za kikristu, kwa ajili ya kuimarika kwa imani ya kikristu ulimwenguni, kwa ajili ya nchi yetu na muungano kati ya mataifa ndani ya Kristu na Kanisa lake, na kwa ajili ya wokovu wa dunia nzima.

7. Yesu anachomwa kwa mkuki moyoni.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, ukubali kupokea, kwa ajili ya mahitaji ya Kanisa Takatifu na kwa ajili ya malipizi ya dhambi za wanadamu wote, Damu na Maji Takatifu vilivyomwagika kutoka jeraha la Moyo Mtakatifu wa Yesu. Utuhurumie. Damu Takatifu ya Yesu, tone lile la mwisho lililomwagika kutoka katika Moyo wake Mtakatifu, unioshe mimi na wengine wote dhambi zetu zote! Ee Maji kutoka katika Moyo Mtakatifu wa Yesu, unioshe na adhabu zote za dhambi zangu na uizime miale ya moto wa toharani kwa ajili yangu na kwa ajili ya roho zote zilizomo toharani. Amina.

Katika mwaka wa Kanisa wa kiliturjia, mwezi Julai ni wa kuiheshimu Damu Takatifu ya Yesu.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Janet Wambura (Guest) on June 20, 2024

🙏💖🙏 Mungu akufunike na upendo

Elizabeth Mrema (Guest) on June 10, 2024

Nakuombea 🙏

Monica Nyalandu (Guest) on April 21, 2024

🙏💖 Mungu wetu asifiwe

Paul Kamau (Guest) on March 18, 2024

🙏🌟 Mungu akujalie amani

Rose Amukowa (Guest) on March 7, 2024

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Alice Mrema (Guest) on December 21, 2023

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Joyce Mussa (Guest) on December 9, 2023

Mungu akubariki!

James Mduma (Guest) on November 19, 2023

🙏❤️💖 Tumshukuru Mungu kwa yote

Stephen Kikwete (Guest) on June 16, 2023

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Rose Mwinuka (Guest) on April 19, 2023

🙏🌟 Mungu alete amani

Wilson Ombati (Guest) on February 23, 2023

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Thomas Mtaki (Guest) on January 3, 2023

🙏💖 Nakusihi Mungu

Francis Mrope (Guest) on December 27, 2022

🙏✨ Mungu asikie maombi yetu

Mariam Kawawa (Guest) on December 25, 2022

🙏🌟 Mbarikiwe sana

Dorothy Nkya (Guest) on December 20, 2022

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Robert Ndunguru (Guest) on November 26, 2022

🙏❤️💖 Bwana akujalie baraka

Stephen Kikwete (Guest) on November 2, 2022

🙏🙏🙏

Joseph Kitine (Guest) on October 29, 2022

🙏❤️🌟 Asante Mungu kwa uhai

Faith Kariuki (Guest) on October 1, 2022

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Robert Ndunguru (Guest) on August 13, 2022

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

David Nyerere (Guest) on July 25, 2022

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

George Tenga (Guest) on July 5, 2022

🙏❤️💖 Baraka za Mungu ziwe nawe

Betty Cheruiyot (Guest) on April 28, 2022

Dumu katika Bwana.

Raphael Okoth (Guest) on April 21, 2022

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Benjamin Kibicho (Guest) on February 10, 2022

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Stephen Kikwete (Guest) on January 14, 2022

Mwamini katika mpango wake.

Peter Mbise (Guest) on January 8, 2022

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Lucy Kimotho (Guest) on October 15, 2021

Amina

Nancy Kawawa (Guest) on September 15, 2021

🙏❤️ Mungu ni mlinzi wetu

John Malisa (Guest) on August 25, 2021

🙏💖 Asante kwa neema zako Mungu

Susan Wangari (Guest) on July 1, 2021

Sifa kwa Bwana!

Stephen Amollo (Guest) on April 29, 2021

🙏✨❤️ Tumwombe Mungu kila siku

Linda Karimi (Guest) on April 14, 2021

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Wilson Ombati (Guest) on March 8, 2021

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Joyce Aoko (Guest) on February 19, 2021

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Nancy Komba (Guest) on January 18, 2021

🙏✨❤️ Neema za Mungu zikufunike

Lucy Wangui (Guest) on August 18, 2020

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Chris Okello (Guest) on July 26, 2020

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Anna Malela (Guest) on July 3, 2020

Neema na amani iwe nawe.

Peter Mbise (Guest) on June 4, 2020

🙏🌟❤️ Nakuombea heri

Stephen Amollo (Guest) on April 7, 2020

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Grace Minja (Guest) on March 23, 2020

🙏❤️ Mungu akubariki

David Chacha (Guest) on November 26, 2019

Endelea kuwa na imani!

Tabitha Okumu (Guest) on August 9, 2019

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Lydia Wanyama (Guest) on July 20, 2019

🙏💖💫 Mungu ni mwema

Andrew Odhiambo (Guest) on July 9, 2019

Tumaini ni nanga ya roho

Edward Lowassa (Guest) on April 28, 2019

🙏❤️ Mungu ni mkombozi

Patrick Mutua (Guest) on April 6, 2019

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Mariam Hassan (Guest) on February 11, 2019

Mungu ni mwema, wakati wote!

Andrew Mchome (Guest) on December 25, 2018

🙏🌟 Neema za Mungu zisikose

Patrick Akech (Guest) on December 20, 2018

🙏✨ Neema ya Mungu iwe nawe

Grace Wairimu (Guest) on November 28, 2018

🙏💖 Nakushukuru Mungu

Carol Nyakio (Guest) on November 15, 2018

🙏💖✨ Neema yako ni ya kutosha

Mary Njeri (Guest) on October 25, 2018

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Anna Malela (Guest) on October 23, 2018

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Victor Kamau (Guest) on October 9, 2018

🙏🌟 Namuomba Mungu akupiganie

Rose Waithera (Guest) on September 30, 2018

Rehema zake hudumu milele

Catherine Mkumbo (Guest) on September 24, 2018

🙏✨ Mungu atakuinua

Patrick Kidata (Guest) on August 16, 2018

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Peter Mugendi (Guest) on August 14, 2018

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Related Posts

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli ni sala nzuri sana ya kumheshimu huyu Malaika Mkuu pamoja na makun... Read More

SALA YA MTU ALIYEKABILIWA NA MATATIZO MBALIMBALI

SALA YA MTU ALIYEKABILIWA NA MATATIZO MBALIMBALI

Ewe Mtakatifu Yuda Tadei,/ mtume mtukufu na shahidi wa Kristo,/ umesifika pote kwa wepesi wako wa... Read More

SALA MUHIMU ZA MKRISTO ZA KILA SIKU ASUBUHI

SALA MUHIMU ZA MKRISTO ZA KILA SIKU ASUBUHI

SALA YA ASUBUHI

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu,... Read More

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Read More

SALA ZA KUMWABUDU YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA ZA KUMWABUDU YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

Ee Yesu Kristu,/ Bwana wangu na M... Read More

SALA YA KUOMBEA FAMILIA

SALA YA KUOMBEA FAMILIA

Ewe Mungu Mwenyezi, sisi kama familia tunakushukuru kwa zawadi ya Mama Kanisa Katoliki ambaye sik... Read More

KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

Ee Mt. Yosefu, Baba Mlishi wa Mwokozi wangu, na mchumba safi wa Mama wa Mungu, leo ninakuchagua w... Read More

SALA YA KUMWOMBA MTAKATIFU TERESIA WA MTOTO YESU

SALA YA KUMWOMBA MTAKATIFU TERESIA WA MTOTO YESU

Ee Mtakatifu Teresia wa mtoto Yesu, ulistahili kuitwa Msimamizi wa misioni katoliki za dunia yote... Read More

ATUKUZWE BABA

ATUKUZWE BABA

Atukuzwe Baba
na Mwana
na Roho Mtakatifu
Kama mwanzo
na sasa,
na siku zo... Read More

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

Ee Yesu Mfungwa wa Upendo wa Mungu,/ ninapofikiri Upendo wako na jinsi ulivyojitolea kwa ajili ya... Read More

LITANIA YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

LITANIA YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie ... Read More

Majitoleo ya asubuhi kwa Bikira Maria

Majitoleo ya asubuhi kwa Bikira Maria

Ee Yesu, kupitia mikono safi ya Bikira Maria, na kwa maungano na sadaka yako kuu, ninakutolea sal... Read More

📘 About 🔒 Login 📝 Register 📞 Contact