Sidebar with Floating Button
MHUBIRI
☰
AckyShine

SALA YA KUOMBEA FAMILIA

Featured Image

Ewe Mungu Mwenyezi, sisi kama familia tunakushukuru kwa zawadi ya Mama Kanisa Katoliki ambaye siku zote hutupatia malezi bora kwa ajili ya wokovu wetu. Kanisa halichoki kutuhimiza tutafakari na kuishi utakatifu wa familia ya Nazareti ya Yesu, Maria na Yosefu. Familia hii iliishi upendo uliojengwa kwa fadhila za imani, uaminifu, utii, uvumilivu na upole hata wakawa watakatifu. Tunapoadhimisha mwaka wa Familia, tunaiweka mbele yetu familia ya Nazareti iwe dira, baraka na mfano kwa familia zetu.

Tunakushukuru Baba kwa ajili ya familia zote zinazojitahidi kuishi fadhila hizo za Familia takatifu na tunakuomba uzidi kuwaimarisha wanandoa ili tupate kwao mifano mingi na bora ya kuigwa. Ee Bwana, tunaomba Roho Mtakatifu atuangazie tuweze: kutambua familia kuwa Kanisa la nyumbani na shule ya imani na upendo; kuimarisha familia kwa sala, sakramenti na tunu za kiinjili na kushirikiana kwa heshima katika familia kwa usitawi wa roho na wa mwili kwa wanafamilia wote.

Tunaziombea familia zetu na Jumuiya Ndogondogo za Kikristo ziwe bustani bora na salama za kuchipusha na kulea miito mitakatifu ya Ndoa, Utawa na Upadre. Tunawaombea vijana na watoto wetu Uchaji wa Mungu ili wawe na bidii ya kujitunza kwa kushika amri za Mungu na kuishi fadhila za kiinjili, wawe na roho ya kimisionari yaani walipende Kanisa na kuwa na moyo wa kueneza ufalme wako kwa matendo ya imani. Baba wa huruma, tunakukabidhi familia zenye misukosuko ya mafarakano, ulevi, ubinafsi, uregevu-dini, uvivu, ushirikina, hofu, magonjwa sugu na mengineyo yenye kuleta huzuni; kwa hisani yako uwape neema, mwanga na nguvu za kuanza maisha mapya yenye amani, waweze kufurahia upatanisho na uponyi wa pendo lako la kibaba kati yao.

Tunaomba toba na msamaha kwa ukatili, manyanyaso na hata mauaji katika familia zetu na uwaponye wote waliojeruhiwa kwa maneno, matendo na makwazo ya aina yeyote. Aidha tunakuomba uwe kitulizo na faraja kwa wagonjwa na wazee, pia tegemeo la yatima na wajane. Wenye matatizo ya kiafya au ya kijamii wasikate tamaa bali waunganishe hali zao na msalaba wa Mwanao na kukutumaini wewe Mweza yote. Jamii iwajibike nao kwa kuzijali haki zao na kuwapa misaada wanayohitaji.

Tunakuomba ubariki miradi na kazi zetu ili familia zipate usitawi na maendeleo; na utujalie hekima ya kukushukuru kwa maisha ya haki, amani na ukarimu na mwisho tukaimbe sifa zako pamoja na familia Takatifu ya Yesu, Maria na Yosefuna jeshi lote la mbinguni. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.

Baba yetu… …..Salamu Maria….…Atukuzwe Baba………

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Edward Chepkoech (Guest) on July 14, 2024

πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike

Mary Mrope (Guest) on April 30, 2024

πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri

Mary Kendi (Guest) on March 13, 2024

πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu

Carol Nyakio (Guest) on January 14, 2024

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Benjamin Kibicho (Guest) on October 20, 2023

πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote

Mariam Kawawa (Guest) on September 17, 2023

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Victor Sokoine (Guest) on September 14, 2023

πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

Stephen Mushi (Guest) on August 31, 2023

Dumu katika Bwana.

Mariam Kawawa (Guest) on July 1, 2023

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Margaret Mahiga (Guest) on June 19, 2023

Nakuombea πŸ™

Anna Mchome (Guest) on May 25, 2023

Neema ya Mungu inatosha kwako

Miriam Mchome (Guest) on April 24, 2023

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Rose Kiwanga (Guest) on March 21, 2023

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Mary Njeri (Guest) on March 12, 2023

Tumaini ni nanga ya roho

David Nyerere (Guest) on November 27, 2022

πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku

Andrew Odhiambo (Guest) on November 2, 2022

πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako

Francis Mtangi (Guest) on October 6, 2022

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

George Mallya (Guest) on May 12, 2022

πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu

Anna Sumari (Guest) on April 17, 2022

Endelea kuwa na imani!

Carol Nyakio (Guest) on March 15, 2022

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Stephen Mushi (Guest) on February 1, 2022

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Irene Akoth (Guest) on December 22, 2021

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Mercy Atieno (Guest) on December 10, 2021

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Ruth Kibona (Guest) on November 7, 2021

Mungu akubariki!

Dorothy Majaliwa (Guest) on November 6, 2021

Neema na amani iwe nawe.

Nancy Kawawa (Guest) on August 27, 2021

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

Benjamin Kibicho (Guest) on June 23, 2021

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

John Lissu (Guest) on April 13, 2021

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Daniel Obura (Guest) on February 14, 2021

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Patrick Kidata (Guest) on February 9, 2021

πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka

Elizabeth Mrema (Guest) on January 6, 2021

Nguvu hutoka kwa Bwana

Joseph Kitine (Guest) on December 8, 2020

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

George Tenga (Guest) on December 1, 2020

πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana

Mary Sokoine (Guest) on November 11, 2020

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Elijah Mutua (Guest) on August 23, 2020

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Nancy Kawawa (Guest) on August 2, 2020

πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu

Stephen Kangethe (Guest) on July 18, 2020

πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu

Charles Mboje (Guest) on May 7, 2020

Amina

Monica Nyalandu (Guest) on April 20, 2020

Mungu ni mwema, wakati wote!

Mary Mrope (Guest) on March 6, 2020

πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo

Sarah Mbise (Guest) on February 18, 2020

Rehema hushinda hukumu

Christopher Oloo (Guest) on August 24, 2019

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Elizabeth Malima (Guest) on June 29, 2019

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Jane Muthui (Guest) on May 24, 2019

Mwamini katika mpango wake.

Linda Karimi (Guest) on April 30, 2019

πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema

Martin Otieno (Guest) on March 21, 2019

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Robert Okello (Guest) on March 10, 2019

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Anna Mahiga (Guest) on February 27, 2019

πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua

Nancy Kawawa (Guest) on November 27, 2018

πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha

Joyce Mussa (Guest) on November 7, 2018

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Rose Kiwanga (Guest) on October 27, 2018

πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi

David Ochieng (Guest) on October 20, 2018

πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu

Ann Wambui (Guest) on October 13, 2018

Katika imani, yote yanawezekana

Nora Lowassa (Guest) on May 28, 2018

πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu

Rose Amukowa (Guest) on April 15, 2018

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Agnes Sumaye (Guest) on January 13, 2018

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Joyce Nkya (Guest) on January 5, 2018

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Grace Majaliwa (Guest) on November 14, 2017

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Richard Mulwa (Guest) on November 6, 2017

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Jacob Kiplangat (Guest) on November 2, 2017

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Related Posts

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

Kwa nguvu zangu zote za moyo wangu/ ninakuabudu ee Moyo Mtakatifu/ na Mwabudiwa sana,/ Moyo Mtaka... Read More

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji ... Read More

Kuweka nia njema

Kuweka nia njema

Kumheshimu Mungu wangu, Namtolea roho yangu, Nifanye kazi nipumzike, Amri zake tu nishike, Wazo n... Read More

Sala fupi ya Asubuhi

Sala fupi ya Asubuhi

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, milele na milele, Amina... Read More

SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI

SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI

Mtakatifu Yuda Tadei,/ Mtume Mtakatifu,/ mtumishi mwaminifu na rafiki wa Yes... Read More

Kanuni ya imani

Kanuni ya imani

Nasadiki kwa Mungu, Baba Mwenyezi,/ mwumba mbingu na dunia./ Na kwa Yesu Kristu, Mwanaye wa pekee... Read More

Sala ya Usiku kabla ya kulala

Sala ya Usiku kabla ya kulala

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

SALA YA KUSHUKURU

Tunakus... Read More

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

Nakusikitikia sana Mama Mtakatifu Maria kwa sababu ya ukiwa wako mkuu. Uchungu wako ulikuwa mkubw... Read More

SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu, utulinde katika vita, uwe kinga yetu katika maovu na maoteo ya sh... Read More

SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE

SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE

Ee Mama mbarikiwa na Bikira mwenye uchungu, Malkia wa Mashahidi, uliyesimama chini ya msalaba na ... Read More

LITANIA YA BIKIRA MARIA MAMA WA MATESO

LITANIA YA BIKIRA MARIA MAMA WA MATESO

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie B... Read More

SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU

SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU

Sali Atukuzwe 7 kwa heshima ya Malaika 7 wateule ujipatie neema ya kuepa dhambi mbaya saba na kut... Read More

πŸ“˜ About πŸ”’ Login πŸ“ Register πŸ“ž Contact