Namna ya kusali Rozari kwa Bikira Maria Mama wa Msaada wa Daima
(Tumia rosari ya kawaida)
Mwanzo, kwenye Msalaba:
Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.
Kwenye chembe ndogo za awali:
K: Ee Mungu utuelekezee msaada W: Ee Bwana utusaidie hima
W: Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu,
Kama mwanzo na sasa na siku zote na milele. Amina.
Maria ametusaidia,
Maria anataka kutusaidia,
Maria anaweza kutusaidia,
Maria atatusaidia.
KATIKA KILA FUNGU SALI SALA ZIFUATAZO:
Kwenye chembe kubwa:
Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu,
Kama mwanzo na sasa, na siku zote, na milele. Amina.
Maria ametusaidia,
Maria anataka kutusaidia,
Maria anaweza kutusaidia,
Maria atatusaidia.
Ee Maria Mama wa Msaada wa daima
Sikiliza maombi ya roho zetu
Unaweza kutusaidia katika mahitaji yetu
Ee Maria kwa matumaini twakuita wewe.
Kwenye chembe ndogo:
Kama unasali mwenyewe: “Ee Maria, utusaidie! (mara kumi)
Kama mnasali zaidi ya mmoja kwa pamoja: K; Ee Maria, W: Utusaidie. (mara kumi)
MWISHO SALI SALA ZIFUATAZO:
Salamu Maria
Salamu Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu, sasa, na saa ya kufa kwetu. Amina. (mara tatu)
Tunaukimbilia
Tunaukimbilia ulinzi wako, ee Mzazi Mtakatifu wa Mungu, usitunyime tukiomba katika shida zetu, utuokoe siku zote, kila tuingiapo hatarini, ee Bikira Mtukufu na mwenye baraka,. Amina.
Agnes Lowassa (Guest) on September 20, 2017
🙏❤️✨ Mungu akujalie furaha
Anna Malela (Guest) on September 6, 2017
🙏❤️✨ Asante Mungu kwa kila kitu
John Malisa (Guest) on August 23, 2017
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Sarah Karani (Guest) on August 19, 2017
🙏🌟❤️ Nakuombea heri
Anna Mahiga (Guest) on June 24, 2017
Neema na amani iwe nawe.
Richard Mulwa (Guest) on June 22, 2017
Imani inaweza kusogeza milima
Samuel Were (Guest) on March 25, 2017
🙏💖 Asante kwa neema zako Mungu
Victor Sokoine (Guest) on March 16, 2017
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
John Malisa (Guest) on January 3, 2017
🙏❤️💖 Baraka za Mungu ziwe nawe
Edith Cherotich (Guest) on December 4, 2016
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Bernard Oduor (Guest) on December 4, 2016
🙏✨ Mungu asikie maombi yetu
Moses Kipkemboi (Guest) on September 4, 2016
🙏✨❤️ Neema za Mungu zikufunike
Anna Mchome (Guest) on August 21, 2016
🙏❤️ Mungu ni mkombozi
Joseph Kitine (Guest) on August 19, 2016
Nakuombea 🙏
Peter Mbise (Guest) on May 10, 2016
🙏🌟 Mungu alete amani
Samuel Omondi (Guest) on February 26, 2016
Endelea kuwa na imani!
Alice Jebet (Guest) on January 16, 2016
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Diana Mallya (Guest) on December 31, 2015
🙏✨ Mungu atakuinua
Robert Okello (Guest) on October 8, 2015
🙏❤️ Mungu ni mlinzi wetu
John Lissu (Guest) on July 31, 2015
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Catherine Mkumbo (Guest) on May 29, 2015
Neema ya Mungu inatosha kwako
Joseph Njoroge (Guest) on May 9, 2015
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Sarah Mbise (Guest) on April 17, 2015
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika