Kijana mmoja alisafiri kwa meli na rafiki zake,
wakiwa katikati ya safari yao meli ilianza
kuzama. Watu wengi pamoja na rafiki wa yule
kijana walikufa maji wakati wanajaribu kujiokoa
kwa kuogelea, lakini yule kijana alifanikiwa
kushika ubao ulioelea majini akaanza kuelea nao,
maji yalimpeleka hadi kisiwa cha mbali sana
ambako hakukuwa na watu wala wanyama
isipokuwa wadudu tu! Alifika ufukweni amechoka
sana na asiyeamini tukio lililotokea, akaishi huko
kwa kula matunda. Aliweza kujenga ka-kibanda
kwa shida sana maana hakuwa na shoka wala
panga, hatimaye akaanza maisha mapya.
Aliishi muda mrefu kisiwani na tayari alishazoea
mazingira yale ya shida japo shida haizoeleki.
Mara zote nyakati za jioni aliwasha moto kwa
kupekecha vijiti. Siku moja kama kawaida yake
aliwasha moto nje karibu na kibanda chake, aliota
moto muda mrefu hatimaye akapitiwa na usingizi.
Alilala hapo hapo hadi usiku wa manane
aliposhtushwa na joto kali lisilo la kawaida.
Kumbe moto ulishika nyasi za kibanda chake na
kibanda chote kikaungua moto.Alilia sana na
kumlaani sana Mungu kwa mateso hayo akisema
"Hivi Mungu nimekukosea nini mpaka unitese
hivi? Pamoja na shida zote hizi bado
unaniongezea shida nyingine, umeteketeza makazi
yangu ilhali nimejenga kwa shida, Hukuridhika
kunitenga mbali na familia yangu nilipoishi kwa
raha? Hukuridhika kuwaua rafiki zangu wote
baharini? Kwanini Mungu umekuwa mkatili hivi?
Bora nife tuu maana nimeshachoshwa na hizi
shida!" akaendelea kulalamika na kumlaani Mungu
hadi kukapambazuka.
Ilipofika asubuhi aliiona meli ikija kwa mbali
kuelekea alipo, alishangaa maana hakuna meli
yoyote inayoweza kwenda kisiwa kile labda kama
imepotea njia. Meli ilipofika ufukweni yule kijana
akaifuata, alienda moja kwa moja hadi kwa
kapteni.Kapteni akamwambia "tuliona moto mkali
sana usiku tukahisi ni meli inawaka moto
tukasema tuje ili tutoe msaada..kwa kweli
tumetembea masaa mengi sana hadi kufika hapa,
mshukuru Mungu maana ametumia moto kutuleta
hapa" yule kijana kusikia hivyo alilia sana,
akajilaumu kwa jinsi alivyo mnung'unikia Mungu.
Akaelewa kuwa Mungu ana njia nyingi za kuleta
msaada kwa mtu. Akapiga magoti akatubu huku
akimshukuru Mungu. Safari ya kurudi nyumbani
ikaanza.
FUNDISHO: Wakati mwingine Kuna mambo
mabaya huwa yanatokea katika maisha yetu
yanayotufanya tuone kama Mungu ametusahau.
Tunamnung'unikia na kumlaumu Mungu bila
kujua kuwa Mungu ana njia nyingi sana kutuletea
msaada. Njia za Mungu huwa zinaonekana kama
ujinga fulani, lakini kiukweli ujinga wa Mungu
ndiyo akili kubwa ya mwisho ya mwanadamu.
Tunasahau kuwa mabaya tunayokutana nayo
yanafanya kazi kwa Manufaa ya hatma zetu.
Unaweza fukuzwa kazi usijue kumbe ndio
unaelekea katika kazi bora zaidi, unaweza
kuachwa na mtu uliyempenda sana ukadhani
ndiyo mwisho wa maisha kumbe Mungu
amekuandalia mtu mwingine mwenye mapenzi ya
dhati mtakayefikia malengo ya kujenga familia,
unaweza kukataliwa na kutengwa na ndugu
kumbe Mungu amekuandalia watu-baki
watakaofanikisha ufikie malengo yako pasipo
masimango ya ndugu, hata rafiki wanaweza
kukusaliti kumbe Mungu amewaondoa makusudi
ili kukuepusha na mabaya waliyoyapanga juu
yako. Sasa usimlaumu Mungu ukadhani
anakuzidishia matatizo, hapo anatafuta njia ya
kuyaondoa hayo matatizo.
Mshukuru Mungu kwa Kila Jambo, kwakuwa
hajawahi kukuwazia mabaya. Anakuwazia mema
sikuzote.
Tafadhari Share kama umeipenda na marafiki
zako wajifunze…….
Sharon Kibiru (Guest) on July 6, 2024
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Andrew Mahiga (Guest) on May 14, 2024
Dumu katika Bwana.
Mary Kidata (Guest) on April 21, 2024
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Monica Adhiambo (Guest) on January 15, 2024
Imani inaweza kusogeza milima
Mary Mrope (Guest) on January 7, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
David Sokoine (Guest) on January 6, 2024
Mungu ni mwema, wakati wote!
Francis Njeru (Guest) on September 30, 2023
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Lydia Wanyama (Guest) on March 26, 2023
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Victor Kamau (Guest) on January 25, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
James Kawawa (Guest) on December 10, 2022
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Betty Cheruiyot (Guest) on September 26, 2022
Mungu akubariki!
Josephine Nduta (Guest) on July 7, 2022
Sifa kwa Bwana!
Andrew Odhiambo (Guest) on June 14, 2022
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Grace Mligo (Guest) on April 16, 2022
Neema ya Mungu inatosha kwako
Jackson Makori (Guest) on December 6, 2021
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Alice Jebet (Guest) on November 17, 2021
Rehema hushinda hukumu
Jane Muthui (Guest) on August 29, 2021
Mwamini katika mpango wake.
Monica Nyalandu (Guest) on March 29, 2021
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Joseph Kiwanga (Guest) on November 20, 2020
Rehema zake hudumu milele
Patrick Kidata (Guest) on November 18, 2020
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Nora Lowassa (Guest) on October 15, 2020
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Lydia Wanyama (Guest) on September 3, 2020
Endelea kuwa na imani!
Victor Mwalimu (Guest) on February 22, 2020
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Anna Malela (Guest) on February 4, 2020
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Ruth Mtangi (Guest) on January 2, 2020
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Agnes Lowassa (Guest) on September 30, 2019
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Lucy Mushi (Guest) on July 11, 2019
Katika imani, yote yanawezekana
Benjamin Masanja (Guest) on June 19, 2019
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Ann Wambui (Guest) on March 26, 2019
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
George Wanjala (Guest) on January 4, 2019
Mwamini Bwana; anajua njia
Simon Kiprono (Guest) on December 19, 2018
Tumaini ni nanga ya roho
Elizabeth Mrope (Guest) on November 24, 2018
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Rose Lowassa (Guest) on July 6, 2018
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Lydia Mahiga (Guest) on May 30, 2018
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Margaret Anyango (Guest) on March 5, 2018
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Peter Mwambui (Guest) on October 1, 2017
Baraka kwako na familia yako.
Joyce Nkya (Guest) on May 20, 2017
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Wilson Ombati (Guest) on March 6, 2017
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Rose Kiwanga (Guest) on February 9, 2017
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Francis Mrope (Guest) on November 3, 2016
Nguvu hutoka kwa Bwana
Alice Wanjiru (Guest) on October 30, 2016
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Joy Wacera (Guest) on August 6, 2016
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Grace Mligo (Guest) on March 4, 2016
Neema na amani iwe nawe.
Irene Akoth (Guest) on February 18, 2016
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Esther Cheruiyot (Guest) on January 28, 2016
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Ruth Wanjiku (Guest) on November 4, 2015
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Nancy Akumu (Guest) on August 28, 2015
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Grace Wairimu (Guest) on August 4, 2015
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Nicholas Wanjohi (Guest) on July 16, 2015
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Mary Kidata (Guest) on April 9, 2015
Nakuombea 🙏