Sidebar with Floating Button
MHUBIRI
AckyShine

Soma stori hii, unaweza ukajifunza kitu

Featured Image

Kijana mmoja alisafiri kwa meli na rafiki zake,
wakiwa katikati ya safari yao meli ilianza
kuzama. Watu wengi pamoja na rafiki wa yule
kijana walikufa maji wakati wanajaribu kujiokoa
kwa kuogelea, lakini yule kijana alifanikiwa

kushika ubao ulioelea majini akaanza kuelea nao,
maji yalimpeleka hadi kisiwa cha mbali sana
ambako hakukuwa na watu wala wanyama
isipokuwa wadudu tu! Alifika ufukweni amechoka
sana na asiyeamini tukio lililotokea, akaishi huko
kwa kula matunda. Aliweza kujenga ka-kibanda
kwa shida sana maana hakuwa na shoka wala
panga, hatimaye akaanza maisha mapya.
Aliishi muda mrefu kisiwani na tayari alishazoea
mazingira yale ya shida japo shida haizoeleki.
Mara zote nyakati za jioni aliwasha moto kwa
kupekecha vijiti. Siku moja kama kawaida yake
aliwasha moto nje karibu na kibanda chake, aliota
moto muda mrefu hatimaye akapitiwa na usingizi.
Alilala hapo hapo hadi usiku wa manane
aliposhtushwa na joto kali lisilo la kawaida.
Kumbe moto ulishika nyasi za kibanda chake na
kibanda chote kikaungua moto.Alilia sana na
kumlaani sana Mungu kwa mateso hayo akisema
"Hivi Mungu nimekukosea nini mpaka unitese
hivi? Pamoja na shida zote hizi bado
unaniongezea shida nyingine, umeteketeza makazi
yangu ilhali nimejenga kwa shida, Hukuridhika
kunitenga mbali na familia yangu nilipoishi kwa
raha? Hukuridhika kuwaua rafiki zangu wote
baharini? Kwanini Mungu umekuwa mkatili hivi?
Bora nife tuu maana nimeshachoshwa na hizi
shida!" akaendelea kulalamika na kumlaani Mungu
hadi kukapambazuka.
Ilipofika asubuhi aliiona meli ikija kwa mbali
kuelekea alipo, alishangaa maana hakuna meli
yoyote inayoweza kwenda kisiwa kile labda kama
imepotea njia. Meli ilipofika ufukweni yule kijana
akaifuata, alienda moja kwa moja hadi kwa
kapteni.Kapteni akamwambia "tuliona moto mkali
sana usiku tukahisi ni meli inawaka moto
tukasema tuje ili tutoe msaada..kwa kweli
tumetembea masaa mengi sana hadi kufika hapa,
mshukuru Mungu maana ametumia moto kutuleta
hapa" yule kijana kusikia hivyo alilia sana,
akajilaumu kwa jinsi alivyo mnung'unikia Mungu.
Akaelewa kuwa Mungu ana njia nyingi za kuleta
msaada kwa mtu. Akapiga magoti akatubu huku
akimshukuru Mungu. Safari ya kurudi nyumbani
ikaanza.
FUNDISHO: Wakati mwingine Kuna mambo
mabaya huwa yanatokea katika maisha yetu
yanayotufanya tuone kama Mungu ametusahau.
Tunamnung'unikia na kumlaumu Mungu bila
kujua kuwa Mungu ana njia nyingi sana kutuletea
msaada. Njia za Mungu huwa zinaonekana kama
ujinga fulani, lakini kiukweli ujinga wa Mungu
ndiyo akili kubwa ya mwisho ya mwanadamu.
Tunasahau kuwa mabaya tunayokutana nayo
yanafanya kazi kwa Manufaa ya hatma zetu.
Unaweza fukuzwa kazi usijue kumbe ndio
unaelekea katika kazi bora zaidi, unaweza
kuachwa na mtu uliyempenda sana ukadhani
ndiyo mwisho wa maisha kumbe Mungu
amekuandalia mtu mwingine mwenye mapenzi ya
dhati mtakayefikia malengo ya kujenga familia,
unaweza kukataliwa na kutengwa na ndugu
kumbe Mungu amekuandalia watu-baki
watakaofanikisha ufikie malengo yako pasipo
masimango ya ndugu, hata rafiki wanaweza
kukusaliti kumbe Mungu amewaondoa makusudi
ili kukuepusha na mabaya waliyoyapanga juu
yako. Sasa usimlaumu Mungu ukadhani
anakuzidishia matatizo, hapo anatafuta njia ya
kuyaondoa hayo matatizo.
Mshukuru Mungu kwa Kila Jambo, kwakuwa
hajawahi kukuwazia mabaya. Anakuwazia mema
sikuzote.
Tafadhari Share kama umeipenda na marafiki
zako wajifunze…….

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Sharon Kibiru (Guest) on July 6, 2024

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Andrew Mahiga (Guest) on May 14, 2024

Dumu katika Bwana.

Mary Kidata (Guest) on April 21, 2024

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Monica Adhiambo (Guest) on January 15, 2024

Imani inaweza kusogeza milima

Mary Mrope (Guest) on January 7, 2024

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

David Sokoine (Guest) on January 6, 2024

Mungu ni mwema, wakati wote!

Francis Njeru (Guest) on September 30, 2023

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Lydia Wanyama (Guest) on March 26, 2023

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Victor Kamau (Guest) on January 25, 2023

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

James Kawawa (Guest) on December 10, 2022

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Betty Cheruiyot (Guest) on September 26, 2022

Mungu akubariki!

Josephine Nduta (Guest) on July 7, 2022

Sifa kwa Bwana!

Andrew Odhiambo (Guest) on June 14, 2022

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Grace Mligo (Guest) on April 16, 2022

Neema ya Mungu inatosha kwako

Jackson Makori (Guest) on December 6, 2021

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Alice Jebet (Guest) on November 17, 2021

Rehema hushinda hukumu

Jane Muthui (Guest) on August 29, 2021

Mwamini katika mpango wake.

Monica Nyalandu (Guest) on March 29, 2021

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Joseph Kiwanga (Guest) on November 20, 2020

Rehema zake hudumu milele

Patrick Kidata (Guest) on November 18, 2020

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Nora Lowassa (Guest) on October 15, 2020

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Lydia Wanyama (Guest) on September 3, 2020

Endelea kuwa na imani!

Victor Mwalimu (Guest) on February 22, 2020

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Anna Malela (Guest) on February 4, 2020

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Ruth Mtangi (Guest) on January 2, 2020

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Agnes Lowassa (Guest) on September 30, 2019

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Lucy Mushi (Guest) on July 11, 2019

Katika imani, yote yanawezekana

Benjamin Masanja (Guest) on June 19, 2019

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Ann Wambui (Guest) on March 26, 2019

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

George Wanjala (Guest) on January 4, 2019

Mwamini Bwana; anajua njia

Simon Kiprono (Guest) on December 19, 2018

Tumaini ni nanga ya roho

Elizabeth Mrope (Guest) on November 24, 2018

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Rose Lowassa (Guest) on July 6, 2018

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Lydia Mahiga (Guest) on May 30, 2018

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Margaret Anyango (Guest) on March 5, 2018

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Peter Mwambui (Guest) on October 1, 2017

Baraka kwako na familia yako.

Joyce Nkya (Guest) on May 20, 2017

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Wilson Ombati (Guest) on March 6, 2017

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Rose Kiwanga (Guest) on February 9, 2017

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Francis Mrope (Guest) on November 3, 2016

Nguvu hutoka kwa Bwana

Alice Wanjiru (Guest) on October 30, 2016

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Joy Wacera (Guest) on August 6, 2016

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Grace Mligo (Guest) on March 4, 2016

Neema na amani iwe nawe.

Irene Akoth (Guest) on February 18, 2016

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Esther Cheruiyot (Guest) on January 28, 2016

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Ruth Wanjiku (Guest) on November 4, 2015

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Nancy Akumu (Guest) on August 28, 2015

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Grace Wairimu (Guest) on August 4, 2015

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Nicholas Wanjohi (Guest) on July 16, 2015

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Mary Kidata (Guest) on April 9, 2015

Nakuombea 🙏

Related Posts

Je, Kanisa Katoliki linamwamini Roho Mtakatifu kama Mungu aliye hai?

Je, Kanisa Katoliki linamwamini Roho Mtakatifu kama Mungu aliye hai?

Je, Kanisa Katoliki linamwamini Roho Mtakatifu kama Mungu aliye hai? Jibu fupi ni ndiyo, Kanisa l... Read More

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha Ubatizo kwa ajili ya ondoleo la dhambi?

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha Ubatizo kwa ajili ya ondoleo la dhambi?

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha Ubatizo kwa ajili ya ondoleo la dhambi?

Ndio,... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu tofauti za kijamii na uadilifu wa kijamii?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu tofauti za kijamii na uadilifu wa kijamii?

Kanisa Katoliki limekuwa likitetea uadilifu wa kijamii na tofauti za kijamii kama sehemu ya imani... Read More

Maana ya Zaka, Sababu za Kutoa Zaka na Faida zake kulingana na Mafundisho ya Kikatoliki, Katekisimu, na Biblia

Maana ya Zaka, Sababu za Kutoa Zaka na Faida zake kulingana na Mafundisho ya Kikatoliki, Katekisimu, na Biblia