Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Mungu Baba wa Mbinguni, Utuhurumie
Mungu Mwana, Mkombozi wa dunia Utuhurumie
Mungu Roho Mtakatifu Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu MMoja Utuhurumie
Maria Mtakatifu Utuombee (iwe kiitikio)
Mama wa Mkombozi wetu,
Mama mwenye mateso,
Malkia wa mashahidi,
Mama wa wenye uchungu,
Mfariji wa wenye taabu,
Msaada wa wenye shida,
Mlinzi wa wenye upweke,
Nguvu ya dhaifu moyoni,
Makimbilio ya wakosefu,
Afya ya wagonjwa,
Matumaini ya wanaozimia,
Kwa ajili ya ufukara wako ulioona pangoni Bethlehemu, - Utusaidie ee Mama wa mateso (iwe kiitikio)
Kwa ajili ya mateso yako uliyoona katika uaguzi wa Simeoni,
Kwa ajili ya taabu zako ulizopata katika safari ya Misri,
Kwa uchungu wako, Mwanao alipopotea,
Kwa ajili ya huzuni yako Mwanao alipodhulumiwa,
Kwa ajili ya hofu yako Yesu alipokamatwa,
Kwa ajili ya uchungu wako ulipokutana na Yesu katika njia ya Msalaba,
Kwa ajili ya mateso ya Moyo wako aliposulibiwa,
Kwa ajili ya mateso yako makali Yesu alipokufa,
Kwa ajili ya kilio chako juu ya Mwanao mpenzi,
Kwa ajili ya uchungu wako penye kaburi la Mwanao,
Kwa ajili ya upweke wako baada ya maziko ya Mwanao,
Kwa ajili ya uvumilivu wako katika shida zote,
Katika uchungu wetu wote,
Katika ugonjwa na mateso,
Katika huzuni na shida,
Katika umaskini na upweke,
Katika mahangaiko na hatari,
Katika vishawisho vyote,
Katika saa ya kifo chetu,
Katika hukumu ya mwisho,
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusikilize ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utuhurumie.
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Bwana utuhurumie – Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie.
Baba Yetu ….
Utuombee, ee Mama wa Mateso
Tujaliwe kupewa ahadi za Kristo.
TUOMBE: Ee Bwana Yesu Kristo, utusaidie sasa na saa ya kifo chetu msaada wa Bikira Maria Mama yako, ambaye moyo wake mtakatifu ulichomwa na upanga wa mateso ulipoteswa na kufa msalabani. Unayeishi na kutawala milele na milele. Amina.
Violet Mumo (Guest) on April 20, 2017
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Richard Mulwa (Guest) on April 15, 2017
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Ann Wambui (Guest) on February 2, 2017
ðŸ™ðŸŒŸâ¤ï¸ Nakuombea heri
Robert Ndunguru (Guest) on January 26, 2017
Katika imani, yote yanawezekana
David Sokoine (Guest) on November 24, 2016
ðŸ™âœ¨â¤ï¸ Tumwombe Mungu kila siku
Mary Kidata (Guest) on November 4, 2016
ðŸ™ðŸ’– Nakushukuru Mungu
David Kawawa (Guest) on October 31, 2016
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Alex Nakitare (Guest) on October 29, 2016
ðŸ™âœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
Lydia Wanyama (Guest) on September 14, 2016
Rehema zake hudumu milele
Robert Okello (Guest) on August 25, 2016
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Violet Mumo (Guest) on August 24, 2016
Tumaini ni nanga ya roho
Elizabeth Mrema (Guest) on May 10, 2016
ðŸ™ðŸŒŸ Mungu akujalie amani
Alex Nakitare (Guest) on April 7, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Joyce Mussa (Guest) on March 9, 2016
ðŸ™â¤ï¸âœ¨ Mungu akujalie furaha
Kenneth Murithi (Guest) on January 25, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Samuel Omondi (Guest) on December 17, 2015
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Mary Mrope (Guest) on November 30, 2015
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
John Lissu (Guest) on November 17, 2015
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Rose Amukowa (Guest) on October 20, 2015
Sifa kwa Bwana!
Lydia Wanyama (Guest) on September 26, 2015
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Joseph Njoroge (Guest) on August 29, 2015
ðŸ™ðŸŒŸ Mbarikiwe sana
Alice Wanjiru (Guest) on August 18, 2015
Rehema hushinda hukumu
Simon Kiprono (Guest) on July 25, 2015
ðŸ™ðŸ’–✨ Neema yako ni ya kutosha