Sidebar with Floating Button
MHUBIRI
☰
AckyShine

SALA YA NOVENA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Featured Image

Ee Moyo Mtakatifu sana wa Yesu, chemchemi ya kila baraka, ninakuabudu, ninakupenda, na kwa majuto halisi ya dhambi zangu, nakutolea moyo wangu dhaifu. Nifanye mnyenyekevu, mvumilivu na safi, nikikubali na kuyatii kabisa mapenzi yako. Ee Yesu mwema, unijalie niishi nawe na kwa ajili yako. Unilinde niwapo katikati ya hatari, unifariji katika mateso, unipe afya ya mwili na msaada katika mahitaji ya mwili, Baraka yako juu ya kila nilifanyalo, na neema ya kifo chema. Amina.

Ee Yesu uliyesema β€œKweli nawaambieni, ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtapata, gongeni nanyi mtafunguliwa”, tazama ninagonga, ninatafuta na kuomba …….. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Yesu uliyesema β€œKweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu mtapewa”, tazama kwa jina lako ninaomba ……. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Yesu uliyesema β€œKweli nawaambieni, mbingu na dunia zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe”, tazama, nikitiwa nguvu na maneno yako ya kweli ninaomba …….. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ambaye kwako ni kitu kimoja tu kisichowezekana, ambacho ni kutoacha kutowaonea huruma wenye huzuni, utuhurumie sisi wakosefu maskini na utujalie neema tukuombayo kwa njia ya Moyo Imakulata wa Maria, Mama yetu mpole.

Sali β€˜Salamu Malkia’ na kuongezea, β€˜Mtakatifu Yosefu Baba Mlishi wa Yesu, utuombee’.

P.S. – Sala hii ya Novena ilisaliwa kila siku na PADRE PIO kwa ajili ya kuwaombea wale wote waliomwomba msaada wa sala zake. Unaweza kuisali kwa namna tofauti tofauti. Mfano, kama Novena ya siku tisa, ambapo unasali sala hii mara moja au zaidi kila siku kwa siku tisa, au unaweza kuifanya kama Novena ya masaa, ambapo unasali sala hii kila baada ya saa moja kwa masaa tisa kwa siku hiyo hiyo, hasa kama kitu unachokiomba ni cha haraka au umesongwa moyoni. Vilevile unaweza kuifanya sala hii kama sehemu ya sala zako za kila siku katika mwezi Juni ambao ni mwezi uliotengwa na Kanisa kwa ajili ya kuuheshimu Moyo Mtakatifu wa Yesu, na hapo utaitumia kuwaombea watu waliokuomba msaada wa sala zako kama alivyofanya Mtakatifu Padre Pio. Pia unaweza kuitumia kama sala yako ya siku zote au ya mara kwa mara kwa ajili ya mahitaji mbalimbali.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Lucy Kimotho (Guest) on September 20, 2017

πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo

Tabitha Okumu (Guest) on August 24, 2017

πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema

Isaac Kiptoo (Guest) on August 13, 2017

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Miriam Mchome (Guest) on July 16, 2017

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Rose Kiwanga (Guest) on June 30, 2017

πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu

James Mduma (Guest) on June 3, 2017

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Rose Kiwanga (Guest) on May 29, 2017

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Christopher Oloo (Guest) on April 30, 2017

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Anna Malela (Guest) on December 5, 2016

πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu

Lydia Mahiga (Guest) on November 14, 2016

πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku

Frank Macha (Guest) on September 8, 2016

πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu

Sarah Karani (Guest) on August 11, 2016

Rehema hushinda hukumu

Charles Mchome (Guest) on August 11, 2016

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Joyce Aoko (Guest) on July 11, 2016

πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie

Diana Mallya (Guest) on April 11, 2016

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Joseph Mallya (Guest) on December 4, 2015

πŸ™πŸ™πŸ™

Hellen Nduta (Guest) on November 5, 2015

Nakuombea πŸ™

Peter Mbise (Guest) on October 23, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Peter Mbise (Guest) on September 23, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Esther Cheruiyot (Guest) on August 25, 2015

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Francis Mrope (Guest) on May 23, 2015

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Nancy Kawawa (Guest) on May 7, 2015

Dumu katika Bwana.

Esther Nyambura (Guest) on April 3, 2015

πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana

Related Posts

SALA ZA KUMWABUDU YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA ZA KUMWABUDU YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

Ee Yesu Kristu,/ Bwana wangu na M... Read More

Sala fupi ya Asubuhi

Sala fupi ya Asubuhi

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, milele na milele, Amina... Read More

SALA YA MTAKATIFU INYASI

SALA YA MTAKATIFU INYASI

Roho ya Kristo unitakase
Mwili wa Kristo uniokoe
Damu ya Kristo unifurahishe
Maji ... Read More

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Anza Novena hii tarehe 19 Agosti ili kumalizia tarehe 27 Agosti na kush... Read More

Sala ya Asubuhi ya kila siku

Sala ya Asubuhi ya kila siku

Kwa jina la Baba….. Ee Baba yetu Mungu mkuu,umenilinda usiku huu. Nakushukuru kwa moyo, ee Baba,M... Read More
SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

Ee Yesu Kristu,/ Bwana wangu na Mungu wangu/ ambaye ninasadiki kuwa upo hapa/ katika Sakramenti T... Read More

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU I

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU I

Utukuzwe ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Uliagua kifo chako./ Katika karamu ya mwisho ulitumia mkate... Read More

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji ... Read More

LITANIA YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

LITANIA YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie ... Read More

SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu, utulinde katika vita, uwe kinga yetu katika maovu na maoteo ya sh... Read More

ATUKUZWE BABA

ATUKUZWE BABA

Atukuzwe Baba
na Mwana
na Roho Mtakatifu
Kama mwanzo
na sasa,
na siku zo... Read More

SALA YA JIONI

SALA YA JIONI

TUNAKUSHUKURU, EE MUNGU KWA MAPAJI YOTE ULIYOTUJALIA LEO AMINA


BABA YETU…………β... Read More

πŸ“˜ About πŸ”’ Login πŸ“ Register πŸ“ž Contact