
Maswali na Majibu kuhusu Karama

Je, karama ni zile za kushangaza tu?
Hapana, karama si zile za kushangaza tu, tena zile muhimu zaidi si hizo, bali zile zinazojenga zaidi Kanisa, kama zile za uongozi:
“Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha” (1Kor 12:28).
“Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema tuliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani; ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake; mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia, kwa bidii; mwenye kurehemu, kwa furaha” (Rom 12:6-8).
Karama nyingine muhimu zinatuwezesha kufanya nini?
Karama nyingine muhimu zinatuwezesha kuishi kwa useja kama Yesu na Paulo, au kwa ndoa:
“Nipendalo ni kwamba watu wote wawe kama mimi nilivyo; walakini kila mtu ana karama yake mwenyewe itokayo kwa Mungu, huyu hivi, na huyu hivi. Lakini nawaambia wale wasiooa bado, na wajane; ni heri wakae kama mimi nilivyo” (1Kor 7:7-8).
“Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa” (Math 19:11).
Tunavyoona katika historia ya watawa, mara nyingi karama ya useja inaendana na nyingine katika maisha ya sala, ya kijumuia na ya kitume. Hivyo Filipo “alikuwa na binti wanne, mabikira, waliokuwa wakitabiri” (Mdo 21:9).
Karama zinagawiwa vipi?
Karama zinagawiwa na Roho Mtakatifu jinsi anavyotaka, si kwa sifa au faida ya binafsi, bali kwa ustawi wa taifa la Mungu.
“Kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye… Je, wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu? Wote wanatenda miujiza? Wote wana karama za kuponya wagonjwa? Wote wanena kwa lugha? Wote wafasiri?… Kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa… Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani” (1Kor 12:11,29-30; 14:12,33). Kwa ajili hiyo mitume walipambanua na kuratibu karama katika ibada na katika maisha ya jumuia zisije zikavuruga Kanisa.
Karama za kushangaza zina hatari gani?
Karama za kushangaza zina hatari mbalimbali, hasa zikitiwa maanani mno. Hapo ni rahisi zilete majivuno, kijicho na mafarakano.
“Ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je, si watu wa tabia ya mwili ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu?… Mmekwisha kushiba, mmekwisha kupata utajiri, mmemiliki pasipo sisi. Naam, laiti mngemiliki… Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke” (1Kor 3:3; 4:8; 10:12).
Katika mambo yasiyothibitika ni rahisi kudanganyika kuwa yametoka kwa Mungu, kumbe sivyo. Kisha kudanganyika ni vigumu kuachana nayo hata yakiwa na madhara kwa mhusika au kwa Kanisa.
“Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani” (1Yoh 4:1).
Tunda la kuongozwa na Roho Mtakatifu ni lipi?
Tunda la kuongozwa na Roho Mtakatifu ni umoja wa Kanisa unaotokana na ustawi wa upendo na vipaji ndani ya waamini.
“Wote walijaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri. Na jamii ya watu walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja” (Mdo 4:31-32).
“Tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria” (Gal 5:22-23).
“Lakini, mkiwa na wivu wenye uchungu na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu, wala msiseme uongo juu ya kweli. Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu, bali ni ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani. Maana hapo palipo wivu na ugomvi, ndipo palipo machafuko, na kila tendo baya. Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi; tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki” (Yak 3:14-17).
Madhehebu yanapozidi kufarakana ni lazima tujiulize kama kweli ni kazi ya Roho Mtakatifu.
Comments
Please log in or register to leave a comment or reply.
Elijah Mutua (Guest) on June 12, 2024
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Anna Kibwana (Guest) on March 16, 2024
Nguvu hutoka kwa Bwana
Nora Lowassa (Guest) on March 6, 2024
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Paul Ndomba (Guest) on September 5, 2023
Baraka kwako na familia yako.
Stephen Amollo (Guest) on April 23, 2023
Neema ya Mungu inatosha kwako
Patrick Akech (Guest) on March 1, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Moses Kipkemboi (Guest) on November 11, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Nicholas Wanjohi (Guest) on July 1, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
Catherine Mkumbo (Guest) on June 22, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Betty Cheruiyot (Guest) on March 27, 2022
Mungu ni mwema, wakati wote!
George Wanjala (Guest) on November 25, 2021
Mwamini katika mpango wake.
David Ochieng (Guest) on April 21, 2021
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Joyce Mussa (Guest) on April 4, 2021
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Joseph Kiwanga (Guest) on January 23, 2021
Imani inaweza kusogeza milima
Elijah Mutua (Guest) on January 20, 2021
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Irene Akoth (Guest) on August 7, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Stephen Malecela (Guest) on May 3, 2020
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Dorothy Nkya (Guest) on April 10, 2020
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Joseph Mallya (Guest) on December 18, 2019
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Joseph Mallya (Guest) on December 16, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
David Musyoka (Guest) on August 9, 2019
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Frank Sokoine (Guest) on August 7, 2019
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
James Kawawa (Guest) on July 6, 2019
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Edward Chepkoech (Guest) on June 29, 2019
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Lydia Mzindakaya (Guest) on June 17, 2019
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
David Ochieng (Guest) on January 29, 2019
Endelea kuwa na imani!
Alex Nyamweya (Guest) on December 31, 2018
Neema na amani iwe nawe.
Violet Mumo (Guest) on August 26, 2018
Mungu akubariki!
Rose Amukowa (Guest) on June 4, 2018
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Sarah Mbise (Guest) on April 15, 2018
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Joseph Kitine (Guest) on April 11, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Alice Jebet (Guest) on April 10, 2018
Nakuombea 🙏
Jane Malecela (Guest) on February 16, 2018
Rehema hushinda hukumu
Stephen Mushi (Guest) on November 4, 2017
Katika imani, yote yanawezekana
Patrick Akech (Guest) on August 8, 2017
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Nancy Kawawa (Guest) on August 5, 2017
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Isaac Kiptoo (Guest) on April 14, 2017
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Samson Tibaijuka (Guest) on March 25, 2017
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Elizabeth Mrope (Guest) on November 28, 2016
Tumaini ni nanga ya roho
Nancy Kawawa (Guest) on November 14, 2016
Dumu katika Bwana.
Faith Kariuki (Guest) on April 25, 2016
Sifa kwa Bwana!
George Wanjala (Guest) on April 1, 2016
Kwa Mungu, yote yanawezekana
John Lissu (Guest) on February 14, 2016
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Henry Mollel (Guest) on January 14, 2016
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Victor Malima (Guest) on November 18, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Ruth Kibona (Guest) on November 6, 2015
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Betty Kimaro (Guest) on July 3, 2015
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Frank Sokoine (Guest) on June 8, 2015
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Catherine Naliaka (Guest) on May 16, 2015
Rehema zake hudumu milele
Janet Wambura (Guest) on April 21, 2015
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha