Sidebar with Floating Button
MHUBIRI
AckyShine

Maswali na Majibu kuhusu Karama

Featured Image
Je, karama ni zile za kushangaza tu?

Hapana, karama si zile za kushangaza tu, tena zile muhimu zaidi si hizo, bali zile zinazojenga zaidi Kanisa, kama zile za uongozi:

“Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha” (1Kor 12:28).

“Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema tuliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani; ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake; mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia, kwa bidii; mwenye kurehemu, kwa furaha” (Rom 12:6-8).







Karama nyingine muhimu zinatuwezesha kufanya nini?

Karama nyingine muhimu zinatuwezesha kuishi kwa useja kama Yesu na Paulo, au kwa ndoa:

“Nipendalo ni kwamba watu wote wawe kama mimi nilivyo; walakini kila mtu ana karama yake mwenyewe itokayo kwa Mungu, huyu hivi, na huyu hivi. Lakini nawaambia wale wasiooa bado, na wajane; ni heri wakae kama mimi nilivyo” (1Kor 7:7-8).

“Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa” (Math 19:11).

Tunavyoona katika historia ya watawa, mara nyingi karama ya useja inaendana na nyingine katika maisha ya sala, ya kijumuia na ya kitume. Hivyo Filipo “alikuwa na binti wanne, mabikira, waliokuwa wakitabiri” (Mdo 21:9).







Karama zinagawiwa vipi?

Karama zinagawiwa na Roho Mtakatifu jinsi anavyotaka, si kwa sifa au faida ya binafsi, bali kwa ustawi wa taifa la Mungu.

“Kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye… Je, wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu? Wote wanatenda miujiza? Wote wana karama za kuponya wagonjwa? Wote wanena kwa lugha? Wote wafasiri?… Kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa… Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani” (1Kor 12:11,29-30; 14:12,33). Kwa ajili hiyo mitume walipambanua na kuratibu karama katika ibada na katika maisha ya jumuia zisije zikavuruga Kanisa.







Karama za kushangaza zina hatari gani?

Karama za kushangaza zina hatari mbalimbali, hasa zikitiwa maanani mno. Hapo ni rahisi zilete majivuno, kijicho na mafarakano.

“Ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je, si watu wa tabia ya mwili ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu?… Mmekwisha kushiba, mmekwisha kupata utajiri, mmemiliki pasipo sisi. Naam, laiti mngemiliki… Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke” (1Kor 3:3; 4:8; 10:12).

Katika mambo yasiyothibitika ni rahisi kudanganyika kuwa yametoka kwa Mungu, kumbe sivyo. Kisha kudanganyika ni vigumu kuachana nayo hata yakiwa na madhara kwa mhusika au kwa Kanisa.

“Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani” (1Yoh 4:1).







Tunda la kuongozwa na Roho Mtakatifu ni lipi?

Tunda la kuongozwa na Roho Mtakatifu ni umoja wa Kanisa unaotokana na ustawi wa upendo na vipaji ndani ya waamini.

“Wote walijaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri. Na jamii ya watu walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja” (Mdo 4:31-32).

“Tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria” (Gal 5:22-23).

“Lakini, mkiwa na wivu wenye uchungu na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu, wala msiseme uongo juu ya kweli. Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu, bali ni ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani. Maana hapo palipo wivu na ugomvi, ndipo palipo machafuko, na kila tendo baya. Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi; tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki” (Yak 3:14-17).

Madhehebu yanapozidi kufarakana ni lazima tujiulize kama kweli ni kazi ya Roho Mtakatifu.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Elijah Mutua (Guest) on June 12, 2024

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Anna Kibwana (Guest) on March 16, 2024

Nguvu hutoka kwa Bwana

Nora Lowassa (Guest) on March 6, 2024

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Paul Ndomba (Guest) on September 5, 2023

Baraka kwako na familia yako.

Stephen Amollo (Guest) on April 23, 2023

Neema ya Mungu inatosha kwako

Patrick Akech (Guest) on March 1, 2023

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Moses Kipkemboi (Guest) on November 11, 2022

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Nicholas Wanjohi (Guest) on July 1, 2022

Mwamini Bwana; anajua njia

Catherine Mkumbo (Guest) on June 22, 2022

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Betty Cheruiyot (Guest) on March 27, 2022

Mungu ni mwema, wakati wote!

George Wanjala (Guest) on November 25, 2021

Mwamini katika mpango wake.

David Ochieng (Guest) on April 21, 2021

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Joyce Mussa (Guest) on April 4, 2021

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Joseph Kiwanga (Guest) on January 23, 2021

Imani inaweza kusogeza milima

Elijah Mutua (Guest) on January 20, 2021

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Irene Akoth (Guest) on August 7, 2020

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Stephen Malecela (Guest) on May 3, 2020

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Dorothy Nkya (Guest) on April 10, 2020

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Joseph Mallya (Guest) on December 18, 2019

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Joseph Mallya (Guest) on December 16, 2019

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

David Musyoka (Guest) on August 9, 2019

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Frank Sokoine (Guest) on August 7, 2019

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

James Kawawa (Guest) on July 6, 2019

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Edward Chepkoech (Guest) on June 29, 2019

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Lydia Mzindakaya (Guest) on June 17, 2019

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

David Ochieng (Guest) on January 29, 2019

Endelea kuwa na imani!

Alex Nyamweya (Guest) on December 31, 2018

Neema na amani iwe nawe.

Violet Mumo (Guest) on August 26, 2018

Mungu akubariki!

Rose Amukowa (Guest) on June 4, 2018

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Sarah Mbise (Guest) on April 15, 2018

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Joseph Kitine (Guest) on April 11, 2018

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Alice Jebet (Guest) on April 10, 2018

Nakuombea 🙏

Jane Malecela (Guest) on February 16, 2018

Rehema hushinda hukumu

Stephen Mushi (Guest) on November 4, 2017

Katika imani, yote yanawezekana

Patrick Akech (Guest) on August 8, 2017

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Nancy Kawawa (Guest) on August 5, 2017

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Isaac Kiptoo (Guest) on April 14, 2017

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Samson Tibaijuka (Guest) on March 25, 2017

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Elizabeth Mrope (Guest) on November 28, 2016

Tumaini ni nanga ya roho

Nancy Kawawa (Guest) on November 14, 2016

Dumu katika Bwana.

Faith Kariuki (Guest) on April 25, 2016

Sifa kwa Bwana!

George Wanjala (Guest) on April 1, 2016

Kwa Mungu, yote yanawezekana

John Lissu (Guest) on February 14, 2016

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Henry Mollel (Guest) on January 14, 2016

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Victor Malima (Guest) on November 18, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Ruth Kibona (Guest) on November 6, 2015

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Betty Kimaro (Guest) on July 3, 2015

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Frank Sokoine (Guest) on June 8, 2015

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Catherine Naliaka (Guest) on May 16, 2015

Rehema zake hudumu milele

Janet Wambura (Guest) on April 21, 2015

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Related Posts

Amri ya Pili ya Mungu: Tunakatazwa kuapa bure au uongo kwa Jina la Mungu

Amri ya Pili ya Mungu: Tunakatazwa kuapa bure au uongo kwa Jina la Mungu

Katika amri ya pili ya Mungu tumekatazwa nini?<... Read More

Maswali na Majibu kuhusu Sanamu katika Kanisa Katoliki

Maswali na Majibu kuhusu Sanamu katika Kanisa Katoliki

Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu upendo na huruma?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu upendo na huruma?

Karibu kwenye makala yangu kuhusu imani ya Kanisa Katoliki kuhusu upendo na huruma. Katika kanisa... Read More

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa kutubu na kumgeukia Mungu katika wongofu wa moyo?

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa kutubu na kumgeukia Mungu katika wongofu wa moyo?

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa kutubu na kumgeukia Mungu katika wongofu ... Read More

Mambo ya Msingi unayopaswa kufahamu kuhusu Ekaristi

Mambo ya Msingi unayopaswa kufahamu kuhusu Ekaristi

Read More
Je, Kanisa Katoliki linakiri na kufundisha amri kumi za Mungu kama mwongozo wa maisha ya Kikristo?

Je, Kanisa Katoliki linakiri na kufundisha amri kumi za Mungu kama mwongozo wa maisha ya Kikristo?

Je, Kanisa Katoliki linakiri na kufundisha amri kumi za Mungu kama mwongozo wa maisha ya Kikristo... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu maombi ya watakatifu?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu maombi ya watakatifu?

Karibu kwenye makala hii kuhusu imani ya Kanisa Katoliki kuhusu maombi ya watakatifu. Kwa Wakatol... Read More

Maswali na Majibu kuhusu Sala

Maswali na Majibu kuhusu Sala

Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu toba na wongofu?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu toba na wongofu?

Katika Kanisa Katoliki, toba na wongofu ni sehemu muhimu ya maisha ya Kikristo. Imani yetu inatuf... Read More

Amri ya nne ya Mungu: Kuheshimu Wazazi

Amri ya nne ya Mungu: Kuheshimu Wazazi

Katika Amri ya nne ya Mungu tumeamriwa nini?Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Maandiko Matakatifu?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Maandiko Matakatifu?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Maandiko Matakatifu?

Kanisa Katoliki linaamini kwa... Read More

Maswali na Majibu kuhusu Liturujia

Maswali na Majibu kuhusu Liturujia

Read More