Ufufuko wa wafu maana yake nini?
Ufufuko wa wafu maana yake mwisho wa dunia watu wote watafufuka na miili yao na kwenda nayo katika furaha ya milele au moto wa milele. (Ayu 19:25-26, Mt 22:30-32, Yh 28-29)
Mbinguni ni mahali pa namna gani?
Mbinguni ni makao mema ya heri na furaha (2Kor 5:1, Ufu, 2:17).
Waendao mbinguni ni wale wanaokufa katika hali ya neema ya utakaso na urafiki na Mungu na waliotakaswa kikamilifu
Motoni ni nini?
Motoni ni makao mabaya kwa Shetani walaaniwa wakaapo mbali na Mungu wakiteswa milele. (Mt 25:41, Mik 9:42-43, 1Yoh 14:15)
Uzima wa milele ni nini?
Uzima wa milele ni maisha ya kukaa mbinguni na Mungu yasiyokua na mwisho.
Toharani ni mahali gani?
Toharani ni mahali pa mateso zinakosafishwa roho ambazo hazikutimiza kitubio vizuri baada ya kuungama dhambi. (1Kor 3:15, 1Pet 1:7).
Je, hatuwezi kupunguza mateso ya roho za marehemu waliokwenda toharani?
Ndiyo: twaweza kupunguza hata kuyamaliza kwa kuwasalia na kuwapatia rehema na hasa kwa kuadhimisha Misa kwa ajili yao. (2Mik 12:38-46)
Mambo makuu manne ya mwisho ni yapi?
Mambo hayo ni;
1. Kifo
2. Hukumu
3. Jehanamu (Motoni)
4. Paradiso. (Toharani/Mbinguni)
Je, ufufuko wa Yesu ni muhimu kwetu pia?
Ndiyo, ufufuko wa Yesu ni muhimu kwetu pia, kwa sababu kwa njia yake tu tunatiwa uzima: sasa rohoni kwa kuondolewa dhambi, na siku ya mwisho mwilini pia kwa kufufuliwa.
Mwenyewe alisema, “Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi ajapokufa, atakuwa anaishi; naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele” (Yoh 11:25- 26).
“Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala. Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu” (1Kor 15:20-21).
“Alitolewa kwa ajili ya makosa yetu, na kufufuka ili tupate kuhesabiwa haki” (Rom 4:25).
Je, ni muhimu tujiandae kufa?
Ndiyo, ni muhimu tujiandae kufa wakati wowote na namna yoyote kwa kuishi kitakatifu sasa na kwa kujiombea neema tutakazohitaji saa ya kufa kwetu, tukijua tumewekewa “kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu” (Eb 9:27).
“Katika mambo yako yote uukumbuke mwisho wako, hivyo hutakosa kamwe hata hatima” (YbS 7:36).
“Hamjui yatakayokuwako kesho! Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka” (Yak 4:14).
“Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni” (Math 26:41).
Je, ina thamani machoni pa Bwana mauti ya mtu aliyemcha?
Ndiyo, “ina thamani machoni pa Bwana mauti ya wacha Mungu wake” (Zab 116:15).
Hasa utiifu wa Yesu msalabani umegeuza laana ya kifo iwe baraka kwa waamini wake.
“Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao” (Ufu 14:13).
Je, sisi wanyonge tunaweza kushiriki uzima wa milele wa Mungu?
Ndiyo, sisi wanyonge tunaweza kushiriki uzima wa milele wa Mungu: hapa duniani katika mwanga hafifu wa imani, na kisha kufa katika uangavu wa utukufu usiofifia kamwe. Kwa kuwa lengo la Baba ni kwamba tuungane na Yesu Mwanae kwa uwezo wa Roho Mtakatifu ili tuwe na utukufu wake.
“Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma” (Yoh 17:3).
“Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe. Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa” (2Pet 1:3-4).
Sisi tuliobatizwa tunaitwa “wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo!” (1Yoh. 3:1).
Kwa sababu tumesadiki kwamba “Mungu ni upendo” (1Yoh 4:8) na kwamba “hakuna lisilowezekana kwa Bwana” (Lk 1:37).
“Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, ‘Aba!’ yaani, ‘Baba!’ Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu” (Gal 4:6-7).
Aliyezungumzia moto wa milele ni nani?
Aliyezungumzia moto wa milele ni hasa Yesu: akitufunulia ukuu wa upendo wa Mungu, aliye heri yetu pekee, alituangalisha juu ya hatari ya kutengana naye milele kwa dhambi. Mwenyewe atatoa hukumu hiyo:
“Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake” (Math 25:41).
“Humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki” (Mk 9:48).
“Na moshi wa maumivu yao hupanda juu hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku” (Ufu 14:11).
Toharani maana yake nini?
Toharani maana yake kuna hali ya muda ambayo huruma ya Mungu inawatakasa marehemu waliofariki dunia katika urafiki naye lakini bila ya usafi kamili unaotakiwa kwa kuingia mbinguni. Sisi tunaweza kuharakisha utakaso wao kwa kumtolea Mungu sala na sadaka, hasa ekaristi. Yuda Mmakabayo “alichanga fedha kwa kila mtu jumla drakma elfu mbili, akazipeleka Yerusalemu kutoa sadaka ya dhambi.
Kwa kufanya hivi alitenda vema na kwa haki, kwa kuwa aliukumbuka ufufuo wa wafu. Maana kama asingalitumaini ya kuwa wale waliokufa watafufuka, ingalikuwa kazi bure isiyo na maana kuwaombea wafu. Lakini kwa kuwa aliufikiri utukufu wa thawabu waliowekewa wale wafao katika utauwa, wazo lake lilikuwa takatifu na la kicho. Ndiyo sababu alifanya upatanisho kwa wafu ili wafunguliwe dhambi zao” (2Mak 12:43-46). Imani hiyohiyo iliongoza Wakristo wa kwanza kuwafanyia marehemu ibada ambayo haieleweki vizuri, lakini hailaumiwi na Mtume Paulo: “Kama wafu hawafufuliwi kamwe, kwa nini kubatizwa kwa ajili yao?” (1Kor 15:29).
Je, mwili utakaofufuliwa ni huuhuu tulionao sasa?
Ndiyo, mwili utakaofufuliwa ni huuhuu tulionao sasa, lakini katika hali tofauti: > “hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutokuharibika” (1Kor 15:42).
Siku ya ufufuo “ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika wingu pamoja na nguvu na utukufu mwingi” (Lk 21:27).
“Saa yaja ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuko wa uzima, na waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu” (Yoh 5:28-29).
“Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele” (Math 25:46).
Siku ya ufufuo Kristo mfalme atatuhukumu vipi?
Siku ya ufufuo Kristo mfalme atatuhukumu kwa kudhihirisha misimamo ya watu wote ambao, kwa kupokea au kukataa upendo wa Mungu moyoni mwao, wametenda mema au la.
“Imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo ili kila mtu apokee ijara ya mambo aliyotenda kwa mwili, kadiri alivyopenda, kwamba ni mema au mabaya” (2Kor 5:10).
“Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulikisha yaliyositirika ya giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu” (1Kor 4:5).
“Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake. Na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi; atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto. Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, ‘Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu; kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha; nalikuwa uchi, mkanivika; nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia… Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi’” (Math 25:31-36,40).
“Heri wenye rehema, maana hao watapata rehema” (Math 5:7).
Baada ya hukumu ya mwisho itakuwaje?
Baada ya hukumu ya mwisho, waadilifu watatukuzwa mwili na roho pamoja na Yesu, na ulimwengu pia utageuzwa.
“Kama ilivyo ahadi yake, tunatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake” (2Pet 3:13).
“Na Roho na Bibi arusi wasema, ‘Njoo!’ naye asikiaye na aseme, ‘Njoo!’… Yeye mwenye kuyashuhudia haya asema, ‘Naam, naja upesi’. Amina. Na uje, Bwana Yesu! Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi nyote. Amina” (Ufu 22:17,20-21).
Samuel Were (Guest) on April 15, 2024
Neema na amani iwe nawe.
James Kawawa (Guest) on March 8, 2024
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Nancy Komba (Guest) on January 23, 2024
Nguvu hutoka kwa Bwana
Jackson Makori (Guest) on July 18, 2023
Rehema hushinda hukumu
Ann Awino (Guest) on March 22, 2023
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Edward Chepkoech (Guest) on March 19, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
Henry Sokoine (Guest) on January 1, 2023
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
George Wanjala (Guest) on October 6, 2022
Mungu ni mwema, wakati wote!
Vincent Mwangangi (Guest) on March 26, 2022
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Kevin Maina (Guest) on February 7, 2022
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
David Kawawa (Guest) on January 27, 2022
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Elizabeth Mtei (Guest) on January 16, 2022
Sifa kwa Bwana!
Elizabeth Mrema (Guest) on January 15, 2022
Mungu akubariki!
Charles Mrope (Guest) on November 2, 2021
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Ann Wambui (Guest) on June 20, 2021
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Benjamin Kibicho (Guest) on October 5, 2020
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Nancy Akumu (Guest) on April 18, 2020
Mwamini katika mpango wake.
Moses Mwita (Guest) on January 16, 2020
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Tabitha Okumu (Guest) on December 4, 2019
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Philip Nyaga (Guest) on October 6, 2019
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Lydia Mzindakaya (Guest) on September 18, 2019
Baraka kwako na familia yako.
Peter Mbise (Guest) on September 6, 2019
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Frank Sokoine (Guest) on August 25, 2019
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Edwin Ndambuki (Guest) on June 1, 2019
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
John Mwangi (Guest) on May 2, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Victor Sokoine (Guest) on March 11, 2019
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Victor Sokoine (Guest) on February 9, 2019
Mwamini Bwana; anajua njia
Dorothy Mwakalindile (Guest) on February 7, 2019
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Chris Okello (Guest) on November 13, 2018
Katika imani, yote yanawezekana
James Kawawa (Guest) on October 2, 2018
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Martin Otieno (Guest) on July 4, 2018
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Monica Lissu (Guest) on March 27, 2018
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Alice Mwikali (Guest) on January 14, 2018
Dumu katika Bwana.
Raphael Okoth (Guest) on December 31, 2017
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Betty Akinyi (Guest) on December 31, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Ruth Kibona (Guest) on September 15, 2017
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Francis Mrope (Guest) on June 10, 2017
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Nancy Kabura (Guest) on May 25, 2017
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Ruth Mtangi (Guest) on April 17, 2017
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Ruth Wanjiku (Guest) on September 13, 2016
Neema ya Mungu inatosha kwako
James Malima (Guest) on June 17, 2016
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Esther Cheruiyot (Guest) on April 25, 2016
Rehema zake hudumu milele
Lydia Mzindakaya (Guest) on April 17, 2016
Tumaini ni nanga ya roho
Thomas Mwakalindile (Guest) on April 7, 2016
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Michael Onyango (Guest) on February 2, 2016
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Carol Nyakio (Guest) on January 7, 2016
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Fredrick Mutiso (Guest) on December 2, 2015
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
James Kimani (Guest) on October 31, 2015
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Martin Otieno (Guest) on October 1, 2015
Nakuombea 🙏
Betty Kimaro (Guest) on September 20, 2015
Endelea kuwa na imani!