Sidebar with Floating Button
MHUBIRI
☰
AckyShine

SALA YA MTU ALIYEKABILIWA NA MATATIZO MBALIMBALI

Featured Image

Ewe Mtakatifu Yuda Tadei,/ mtume mtukufu na shahidi wa Kristo,/ umesifika pote kwa wepesi wako wa kutoa misaada/ kwa wanaokukimbilia katika matatizo yao mazito./ Pia ni mwombezi wa waliopondeka moyo./

Mimi ni mmoja wa hao./ Nakujia na moyo uliojaa shida na matatizo./ Nakusihi kwa moyo wote/ unisaidie kwa maombezi yako yenye nguvu/ kufikia utatuzi unaofaa kadiri ya mapenzi ya Mungu./ Maisha yangu yamejaa misalaba,/ siku kwa siku matatizo hayapungui./ Moyo wangu umekuwa bahari ya siki chungu sana./ Mapito yangu nayaona yamejaa miiba mikali./ Roho yangu imezama katika dimbwi la machozi na kite./ Nafsi yangu imezingirwa na giza nene./ Ghasia na kukatishwa tamaa ya kuishi/ hunyemelea roho yangu./ Maongozi ya Mungu na imani naviona vinanitoka kidogo kwa kidogo./

Nikielemewa na mawazo kama hayo/ najikuta sina nguvu za kuishi,/ na maisha kwangu ni msalaba mzito/ ninaouogopa hata kuunyakua./ Wewe unaweza kabisa kunitoa katika balaa hili./ Sitaacha kukusihi/ hadi hapo utakaponisaidia/ au kunijulisha mapenzi ya Mungu kwangu./ Natangulia kutoa shukrani kwa jibu liwalo lote.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Anna Sumari (Guest) on September 20, 2017

πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani

Carol Nyakio (Guest) on September 1, 2017

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Andrew Mahiga (Guest) on May 11, 2017

Neema ya Mungu inatosha kwako

Margaret Mahiga (Guest) on February 8, 2017

πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie

Rose Waithera (Guest) on January 17, 2017

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Philip Nyaga (Guest) on January 12, 2017

Katika imani, yote yanawezekana

David Sokoine (Guest) on October 28, 2016

πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka

Linda Karimi (Guest) on September 28, 2016

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Mariam Kawawa (Guest) on September 16, 2016

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

Joyce Aoko (Guest) on August 25, 2016

Mwamini Bwana; anajua njia

Edward Lowassa (Guest) on August 19, 2016

πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu

Monica Lissu (Guest) on June 27, 2016

Nguvu hutoka kwa Bwana

John Lissu (Guest) on June 10, 2016

πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo

Hellen Nduta (Guest) on April 11, 2016

πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu

Simon Kiprono (Guest) on February 26, 2016

Tumaini ni nanga ya roho

Emily Chepngeno (Guest) on February 2, 2016

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Brian Karanja (Guest) on November 5, 2015

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Mary Mrope (Guest) on October 10, 2015

πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose

Nancy Kabura (Guest) on September 27, 2015

Mwamini katika mpango wake.

Joy Wacera (Guest) on August 5, 2015

πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu

Stephen Kikwete (Guest) on July 29, 2015

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Anna Mahiga (Guest) on July 1, 2015

Wakati wa Mungu ni kamilifu

David Musyoka (Guest) on June 7, 2015

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Related Posts

ROZARI, MATENDO NA LITANI YA MAMA BIKIRA MARIA

ROZARI, MATENDO NA LITANI YA MAMA BIKIRA MARIA

Read More
Sala ya Baba Yetu: Sala ya Bwana

Sala ya Baba Yetu: Sala ya Bwana

Baba Yetu uliye mbinguni,
jina lako litukuzwe;
ufalme wako ufike,
... Read More

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

Ee Bwana Yesu Kristo. Mkombozi wetu, kwa mapendo na tamaa yako ya kutaka kulinda vema Kanisa lako... Read More

Sala ya Saa Tisa

Sala ya Saa Tisa

✝⌚✝

Sala ya saa tisaπŸ™πŸΎ

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu.... Read More

ROSARI YA BIKIRA MARIA MAMA WA MSAADA WA DAIMA

ROSARI YA BIKIRA MARIA MAMA WA MSAADA WA DAIMA

Namna ya kusali Rozari kwa Bikira Maria Mama wa Msaada wa Daima

(Tumia rosari ya kawaida... Read More

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji ... Read More

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU II

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU II

Yesu, Mungu wangu mpenzi,/ upo hapa katika Altare mbele yangu;/ na mimi napiga magoti mbele yako.... Read More

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

Kwa nguvu zangu zote za moyo wangu/ ninakuabudu ee Moyo Mtakatifu/ na Mwabudiwa sana,/ Moyo Mtaka... Read More

SALA YA MATUMAINI

SALA YA MATUMAINI

Mungu wangu,

natumaini kwako nitapewa kwa njia ya Yesu Kristu,

neema zako duniani na ... Read More

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria... Read More

SALA YA MAOMBI KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

SALA YA MAOMBI KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakukimbilia, ninakuja kwako katika mikono yako yenye huruma. Ndiwe ... Read More

Sala ya Usiku kabla ya kulala

Sala ya Usiku kabla ya kulala

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

SALA YA KUSHUKURU

Tunakus... Read More

πŸ“˜ About πŸ”’ Login πŸ“ Register πŸ“ž Contact