Sidebar with Floating Button
MHUBIRI
AckyShine

Maana ya siku ya Jumatano ya Majivu

Featured Image

Utangulizi


Wakati umetimia na ufalme wa Mungu umekaribia, tubuni na kuiamini Injili, (Mk 1:15), haya ndiyo maneno ya kwanza ya Yesu ambayo kadri ya Mwinjili Marko yanafungua kazi ya hadhara ya Yesu, kwa maana hiyo kazi ya Yesu inaanza kwa kuwaandaa watu katika toba ili hatimaye, wapate kuukaribia au kuingia katika ufalme wa Mungu.

Na wakati ndiyo sasa. Wakati ni sasa, Yesu anatuhubiria na Kwaresima imewadia, na ndiyo maana siku ya Jumatano ya majivu, kwa kuitikia mwito wa maneno ya Yesu kanisa linatualika kuingia katika kipindi cha Kwaresma, ambacho ni kipindi cha kujikusanya, kujitayarisha, kijitengeneza na kujikarabati hasa kwa toba, kufunga, kusali na kujitoa sadaka zaidi mambo yanayorutubishwa kwa tafakari ya kina ya Neno la Mungu.

Nini maana ya Jumatano ya majivu?


Jumatano ya majivu ni mwanzo wa kipindi cha kwaresima katika kanisa, Ni mwanzo wa siku arobaini za kutafakari kwa undani fumbo kuu la upendo wa Mungu linalofunuliwa kwa kujitoa kwake na kufa msalabani, kifo cha aibu cha Msalaba ili kuichukua aibu yetu au dhambi zetu.

Kwaresma ni nini?


Kwaresma ni kipindi cha siku 40 cha kujiandaa kuadhimisha Sherehe kuu ya PASAKA yaani kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Tunajiandaa kwa Kufunga Kusali, Kutubu, na Matendo mema.
Mama kanisa anatupatia kipindi hiki ili tuweze kutafakari njia na mienendo yetu na kubadilika kama haimpendezi Mungu

Tunapofunga tunatakiwa kuzuia vilema vyetu na kuviacha kabisa, tunaomba kujaliwa moyo wa toba, tunainua mioyo yetu na tunaomba Mungu atujalie nguvu na tuzo. Haitoshi tu kukiri makosa yetu bali tunahimizwa kuungama na kutubu hayo makosa na kuwa tayari kuanza upya. Kipindi cha Kwaresima huanza tangu Jumatano ya majivu. Mwanzoni mwa kazi yake ya kuhubiri Habari njema Yesu anaanza kwa kusema tubuni na kuiamini Injili – Mk 1,15. Maneno haya haya tunayasikia/tumeyasikia kila tunapopakwa majivu. Mwaliko huu wa Yesu unatuingiza katika kipindi cha toba – tubuni na kuiamini Injili. Huu ni mwaliko wa uzima. Ni mwaliko ili tuongoke, tuanze maisha mapya, maisha ya sala, kufunga na kutoa sadaka.

Kwa nini ikaitwa Jumatano ya majivu?


Jina linatokana na desturi ya kumpaka mtu majivu kichwani pamoja na kumtamkia maneno ya kumhimiza afanye toba inavyotakiwa na kipindi hicho cha liturujia kinachoandaa Pasaka.

Kwa kawaida siku ya Jumatano ya majivu unaanza mfungo unaofuata kielelezo cha Yesu kufunga chakula siku arubaini jangwani baada ya kubatizwa na Yohane Mbatizaji na kabla ya kuanza utume wake mwenyewe.

Nini maana ya majivu tunayopaka?


Majivu ni ishara ya majuto, nayo hufanywa visakramenti kwa kubarikiwa na kanisa. Tunapopakwa majivu katika paji la uso hutusaidia kutafakari na kutukumbusha kuwa wanadamu sisi tu mavumbi na mavumbini tutarudi. Hutukumbusha zaidi kuwa maisha ya hapa duniani tunapita na safari yetu itakamilika pale tutakapoungana na Bwana na mwokozi wetu katika ufalme wako.
Angalia; Isaya 61:3, Ester 4:1-3, Yeremia 6:26, Ezekieli 27:30, Mathayo 11:21 na Luka 10:13.

Kwa nini majivu yanapakwa kwenye paji la uso na si vinginevyo?


Ishara yoyote iwekwayo katika paji la uso huonesha umiliki (soma Ufunuo 7:3, Ufunuo 9:4, Ufunuo 14:1, Ezekieli 9:4-6, ). Tunapochorwa ishara ya msalaba katika paji la uso ni ishara kwamba sisi tupo chini yake yeye aliyekufa msalabani kwa ajili yetu.
Hali kadhalika hutukumbusha ishara ya msalaba tuliyochorwa na mafuta matakatifu siku ya ubatizo wetu, hutukumbusha ahadi tuliyoiweka siku hiyo ya ubatizo na kutuita tuishi maisha ya utakatifu

Padri hutamka maneno gani wakati anapaka majivu?


Tunapopakwa majivu Padre husema; Mwanadamu kumbuka u mavumbi na mavumbini utarudi AU Tubuni na kuiamini Injili.


Maneno anayosema padre yana maana gani?


Maneno haya kwa upande mmoja hutukumbusha tunapoelekea, tusisikitike kwamba siku moja tutarudi mavumbini bali tuwe na furaha kwani wakati miili yetu unarudi mavumbini roho zetu zitakwenda kuungana na Mungu Baba mbinguni.
Hivyo maandalizi tunayoalikwa kuyafanaya si maandalizi ya kuelekea mavumbini bali maandalizi ya kuelekeza roho zetu mbinguni. Ndio maana pia twaambiwa tubuni na kuiamini Injili.

Majivu tunayopakwa yanatoka wapi?


Majivu tunayopakwa hutoka katika matawi yaliyotumika katika jumapili ya matawi ya mwaka jana. Majivu haya hubarikiwa na kuwa visakramenti. Hivyo majivu yanapoashiria toba na majuto pia hutukumbusha wema wa Mungu na utayari wake wa kutusamehe.

Kwa nini unatumia matawi ya Jumapili ya Matawi?


Matawi haya yalimkaribisha Yesu Yerusalemu akiwa tayari kufa kwa ajili ya dhambi zetu, yalimpokea mfalme kwa furaha na shangwe kuu. Matawi haya yanapochomwa na sisi kupakwa majivu yetu yanatukumbusha kuwa ni kwa ajili ya dhambi zetu Mungu alimtoa mwanae wa pekee kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu sisi wanaadamu. Hivyo hututafakarisha kuacha dhambi.

Kanisa limekataza nini siku ya Jumatano ya majivu?


Tumekatazwa kula chakula siku ya Jumatano ya Majivu na kula nyama siku ya Ijumaa Kuu katika Amri ya Pili ya Kanisa.

Nani analazima kufunga siku ya Jumatano ya majivu na Kwaresma?


Kila Mkristo aliyetimiza miaka 14 na zaidi anapaswa kufunga kula nyama (Ijumaa kuu) na mwenye miaka zaidi ya 21 kufunga chakula Jumatano ya Majivu

Tunaposema kujinyima wakati wa Kwaresma tunamaana gani?


Kujinyima ni kujikatalia kitu ukipendacho mfano nyama, pombe, sigara, muziki, safari, maongezi n.k.

Mwisho


Wakati wa Kwaresma Waamini wanapaswa kujitakasa zaidi kwa kusali, kufunga, toba na matendo mema

Kipindi cha Kwaresima ni fursa makini ya kumkimbilia Mwenyezi Mungu, kwani kwa njia ya dhambi wamejikuta wakiwa mbali na Uso wa huruma ya Mungu, kiasi hata cha kupoteza imani na matumaini kwa Mwenyezi Mungu. Hii ni changamoto ya kumpenda Mungu na jirani badala ya kukumbatia malimwengu yanayoendelea kuwatumbukiza katika utupu wa maisha ya kiroho. Kwaresima ni kipindi cha waamini kukimbilia na kuambata huruma ya Mungu inayoganga na kuponya dhambi. Ni wakati wa sala, upendo na kufunga.
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Victor Kimario (Guest) on April 19, 2024

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Janet Sumaye (Guest) on April 6, 2024

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Victor Sokoine (Guest) on January 15, 2024

Mungu ni mwema, wakati wote!

Chris Okello (Guest) on December 27, 2023

Nguvu hutoka kwa Bwana

Hellen Nduta (Guest) on July 4, 2023

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

David Musyoka (Guest) on June 6, 2023

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

George Mallya (Guest) on March 5, 2023

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Ruth Mtangi (Guest) on August 22, 2022

Mwamini Bwana; anajua njia

Kenneth Murithi (Guest) on March 27, 2022

Katika imani, yote yanawezekana

Michael Mboya (Guest) on December 22, 2021

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Stephen Malecela (Guest) on November 23, 2021

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Emily Chepngeno (Guest) on November 1, 2021

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

John Mushi (Guest) on September 18, 2021

Rehema zake hudumu milele

Esther Nyambura (Guest) on August 4, 2021

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Anthony Kariuki (Guest) on July 18, 2021

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Margaret Anyango (Guest) on July 1, 2021

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Grace Wairimu (Guest) on May 4, 2021

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Janet Sumaye (Guest) on April 24, 2021

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

James Malima (Guest) on April 23, 2021

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Elizabeth Mrema (Guest) on April 15, 2021

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Ruth Wanjiku (Guest) on March 3, 2021

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Anna Malela (Guest) on August 20, 2020

Mungu akubariki!

Ruth Kibona (Guest) on June 24, 2020

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Elizabeth Malima (Guest) on August 23, 2019

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Andrew Mchome (Guest) on July 24, 2019

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Nicholas Wanjohi (Guest) on May 10, 2019

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Rose Mwinuka (Guest) on May 8, 2019

Mwamini katika mpango wake.

Nancy Kabura (Guest) on April 19, 2019

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Mariam Hassan (Guest) on April 10, 2019

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Mercy Atieno (Guest) on February 15, 2019

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Henry Mollel (Guest) on February 9, 2019

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Monica Adhiambo (Guest) on January 7, 2019

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Catherine Mkumbo (Guest) on October 17, 2018

Neema na amani iwe nawe.

Stephen Malecela (Guest) on September 23, 2018

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Joseph Kiwanga (Guest) on July 16, 2018

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Peter Mugendi (Guest) on May 6, 2018

Kwa Mungu, yote yanawezekana

James Mduma (Guest) on March 12, 2018

Baraka kwako na familia yako.

George Ndungu (Guest) on November 28, 2017

Sifa kwa Bwana!

Rose Lowassa (Guest) on February 25, 2017

Rehema hushinda hukumu

Victor Malima (Guest) on November 29, 2016

Wakati wa Mungu ni kamilifu

David Sokoine (Guest) on October 4, 2016

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Jane Muthoni (Guest) on August 29, 2016

Neema ya Mungu inatosha kwako

Andrew Mchome (Guest) on May 25, 2016

Dumu katika Bwana.

Robert Ndunguru (Guest) on May 16, 2016

Endelea kuwa na imani!

Joyce Nkya (Guest) on March 4, 2016

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Nancy Komba (Guest) on February 6, 2016

Tumaini ni nanga ya roho

Charles Wafula (Guest) on December 18, 2015

Nakuombea 🙏

Nancy Komba (Guest) on October 24, 2015

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Lydia Mahiga (Guest) on July 3, 2015

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Monica Nyalandu (Guest) on June 12, 2015

Imani inaweza kusogeza milima

Related Posts

Uzinzi na Uasherati ndio mtego wa kizazi hiki

Uzinzi na Uasherati ndio mtego wa kizazi hiki

Uzinzi na uasherati wakati huu umekuwa ndio sumaku kuu ya kuwanasa watu ili waende jehanamu.

<... Read More
Mafundisho Kuhusu Bikira Maria

Mafundisho Kuhusu Bikira Maria

Read More

Mafundisho na mapokeo Katika Kanisa Katoliki yanapopatikana kwenye Biblia

Mafundisho na mapokeo Katika Kanisa Katoliki yanapopatikana kwenye Biblia

Read More
Ibada Kuu ya Huruma ya Mungu: Kupokea Baraka Tele

Ibada Kuu ya Huruma ya Mungu: Kupokea Baraka Tele

Ibada Kuu ya Huruma ya Mungu: Kupokea Baraka Tele

Kama Mkristo, tunaamini kuwa huruma ya M... Read More

Kupokea Huruma ya Mungu: Kuishi kwa Shukrani na Ukarimu

Kupokea Huruma ya Mungu: Kuishi kwa Shukrani na Ukarimu

Kupokea Huruma ya Mungu: Kuishi kwa Shukrani na Ukarimu

Karibu kwenye makala hii ambayo in... Read More

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi uadilifu wa kijamii na kupinga ubaguzi na ukosefu wa haki katika jamii?

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi uadilifu wa kijamii na kupinga ubaguzi na ukosefu wa haki katika jamii?

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi uadilifu wa kijamii na kupinga ubaguzi na ukosefu... Read More

Ibada ya Chaplet ya Huruma ya Mungu: Sala ya Upatanisho na Ukombozi

Ibada ya Chaplet ya Huruma ya Mungu: Sala ya Upatanisho na Ukombozi

Ibada ya Chaplet ya Huruma ya Mungu: Sala ya Upatanisho na Ukombozi

Sala ni njia ya kuwasi... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu haki na haki za binadamu?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu haki na haki za binadamu?

Kanisa Katoliki ni mojawapo ya madhehebu makubwa duniani na linazingatia sana haki na haki za bin... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti ya Kipaimara?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti ya Kipaimara?

Sakramenti ya Kipaimara ni sakramenti ya tatu katika Kanisa Katoliki baada ya Sakramenti ya Ubati... Read More

Ibada ya Jumapili ya Huruma ya Mungu: Kupata Upendo Usiokuwa na Kifani

Ibada ya Jumapili ya Huruma ya Mungu: Kupata Upendo Usiokuwa na Kifani

Karibu kwa Ibada ya Jumapili ya Huruma ya Mungu! Leo tunajikita katika kupata upendo usiokuwa na ... Read More

Je, Kanisa Katoliki linamwamini Roho Mtakatifu kama Mungu aliye hai?

Je, Kanisa Katoliki linamwamini Roho Mtakatifu kama Mungu aliye hai?

Je, Kanisa Katoliki linamwamini Roho Mtakatifu kama Mungu aliye hai? Jibu fupi ni ndiyo, Kanisa l... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu viongozi wa kidini na maaskofu?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu viongozi wa kidini na maaskofu?

Katika imani ya Kanisa Katoliki, viongozi wa kidini na maaskofu ni watu muhimu sana katika kufiki... Read More

📘 About 🔒 Login 📝 Register 📞 Contact