Sidebar with Floating Button
MHUBIRI
AckyShine

Unayopaswa kujua Kuhusu Kipindi cha Majilio

Featured Image
Majilio (pia: Adventi ) ni kipindi cha liturujia ya
madhehebu mbalimbali ya Ukristo (kama vile
Kanisa Katoliki, ya Waorthodoksi , Waanglikana
na Walutheri ) kinatangulia sherehe ya Noeli na
kuanza mwaka wa liturujia. Kinaweza kudumu
kati ya siku 22 na 40.

Jina lake kwa Kilatini ni adventus maana yake
ujio (wa Yesu Kristo ), lakini jina la Kiswahili ni
sahihi zaidi kwa sababu linadokeza kuwa ujio
wa Yesu ni kwa ajili yetu na kuwa alikuja
zamani, anakuja kila siku na atakuja kwa
utukufu mwisho wa dunia.
Maana ya Majilio katika
maisha ya binadamu
Sisi binadamu hatuwezi kuishi daima katika
hali ileile bila ya matazamio. Hasa kijana
anatarajia mambo mapya tena mema. Hivyo
tunajitahidi kuyapata. Asiyetazamia chochote
amevunjika moyo, hana hamu ya kuishi. Lakini
matazamio ya kibinadamu yakimfikia mtu
hayamridhishi moja kwa moja. Kristo tu
anatimiza hamu zote kwa kumkomboa kutoka
unyonge. Majilio yanatukumbusha kila mwaka
matarajio ya kweli na hivyo yanaamsha hamu
ya kuishi kwa bidii ya kiroho.

MAJILIO: Katika Kanisa la Roma.
Katika mwaka wa liturujia ya Kanisa la Roma ,
sherehe ya Noeli inaandaliwa na kipindi cha
Majilio ambacho kina mambo mawili:
kinakumbusha Mwana wa Mungu alivyotujilia
mara ya kwanza, na papo hapo kinatuandaa
kumpokea atakapotujilia tena siku ya mwisho .
Kufuatana na hayo kina sehemu mbili: hadi
tarehe 16 Desemba kinahusu zaidi kurudi kwa
Bwana; siku nane za mwisho kinatuelekeza
moja kwa moja kuadhimisha kuzaliwa kwake.
Urefu wa Majilio unategemea siku
inayoangukia Noeli, kwa kuwa ni lazima yawe
na Jumapili nne. Hivyo basi yanaanza kwa
Masifu ya Jioni ya kwanza ya Jumapili
inayoangukia tarehe 30 Novemba au tarehe ya
jirani zaidi; yanakwisha kabla ya Masifu ya
Jioni ya kwanza ya Noeli.
Kwa jumla ni kipindi cha toba: rangi yenyewe
ni zambarau; haziruhusiwi sherehe za fahari;
ala za muziki na maua vinaweza kutumika
kwa kiasi tu. Masharti hayo yanalegezwa
katika Jumapili ya tatu kwa sababu ya furaha
ya kuona tunakaribia sherehe yenyewe.
Katika kipindi hicho tunaadhimisha tumaini la
Israeli lililotimizwa Yesu alipokuja katika
unyenyekevu wa umbile letu; pia tunangojea
arudi kwa utukufu. Kama alivyotekeleza ahadi
mara ya kwanza, atazitekeleza pia mara ya
pili, ingawa kwake miaka elfu ni kama siku
moja tu. Kati ya majilio hayo mawili, Bwana
anatujilia mfululizo kifumbo katika sakramenti
(hasa ekaristi ) na katika maisha ya kila siku
kwa njia ya matukio na watu (hasa maskini ).
Basi tunapaswa kuwa tayari daima kumpokea
ili siku ya mwisho tukamlaki, naye
atukaribishe kwenye uzima wa milele. Pia
tunapaswa kumuomba aje kutukomboa, yeye
aliye tumaini letu.

Katika safari ya Majilio watu watatu
wanatuongoza tukutane na Yesu:
1. Isaya
nabii wa tumaini, mwenye kipaji cha kutokeza
matazamio ya binadamu na kumhakikishia
atatimiziwa na Mwokozi
. 2. Yohane Mbatizaji ,
mwenye kuhimiza toba kwa kuwa tunapaswa
kupindua maisha yetu ili tukutane vema na
Kristo.
3. Maria , bikira aliyekuwa tayari
kumpokea Masiya kwa upendo na kushirikiana
naye katika kutimiza mpango wa wokovu .
Tukiwafuata hao watatu tunaweza kujipatia
maadili yale yanayotuandaa kumpokea
Mwokozi anapotujilia: ndiyo matunda maalumu
tunayotarajiwa kuyachuma wakati wa Majilio:
1. Kukesha katika imani, sala na kutambua
ishara za Bwana kutujilia katika nafasi yoyote
ya maisha na mwishoni mwa nyakati.
2.Kuongoka kwa kufuata njia nyofu.
3.Kushuhudia furaha inayoletwa na Yesu kwa
kuwa na upole na uvumilivu kwa wenzetu, kwa
tumaini la kuwa bidii zetu zinawahisha ufalme
wa Mungu wenye heri isiyo na mwisho.
4. Kutunza unyenyekevu kwa kufuata mifano ya
maskini wa Injili ambao ndio waliompokea
Mkombozi .

kwa mambo mengi mengine ya dini tembelea
https://ludovicktmedia.blogspot.com/
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Anna Mahiga (Guest) on July 2, 2024

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

George Mallya (Guest) on May 31, 2024

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Paul Kamau (Guest) on March 23, 2024

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Isaac Kiptoo (Guest) on February 3, 2024

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Rose Kiwanga (Guest) on October 30, 2023

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Kenneth Murithi (Guest) on May 18, 2023

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Nancy Akumu (Guest) on December 2, 2022

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Josephine Nekesa (Guest) on October 7, 2022

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

John Mwangi (Guest) on September 28, 2022

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Frank Sokoine (Guest) on May 6, 2022

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Frank Sokoine (Guest) on March 19, 2022

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Charles Mboje (Guest) on July 4, 2021

Mwamini Bwana; anajua njia

Nancy Komba (Guest) on April 17, 2021

Nguvu hutoka kwa Bwana

Charles Mboje (Guest) on January 26, 2021

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Peter Mbise (Guest) on December 2, 2020

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Kenneth Murithi (Guest) on November 22, 2020

Sifa kwa Bwana!

Sarah Karani (Guest) on September 14, 2020

Rehema zake hudumu milele

Lucy Mahiga (Guest) on May 9, 2020

Endelea kuwa na imani!

Grace Majaliwa (Guest) on May 7, 2020

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Rose Lowassa (Guest) on April 30, 2020

Rehema hushinda hukumu

Henry Mollel (Guest) on January 12, 2020

Mungu ni mwema, wakati wote!

Josephine Nekesa (Guest) on September 17, 2019

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Elizabeth Malima (Guest) on May 11, 2019

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Peter Otieno (Guest) on March 27, 2019

Katika imani, yote yanawezekana

John Mwangi (Guest) on March 20, 2019

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Stephen Kikwete (Guest) on January 30, 2019

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Rose Lowassa (Guest) on July 28, 2018

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Mariam Kawawa (Guest) on May 25, 2018

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Joyce Aoko (Guest) on March 19, 2018

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

George Mallya (Guest) on March 19, 2018

Baraka kwako na familia yako.

Alice Mrema (Guest) on February 28, 2018

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Paul Ndomba (Guest) on December 23, 2017

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

James Mduma (Guest) on November 15, 2017

Neema ya Mungu inatosha kwako

Isaac Kiptoo (Guest) on September 11, 2017

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Ann Awino (Guest) on September 2, 2017

Dumu katika Bwana.

Robert Okello (Guest) on May 6, 2017

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Monica Adhiambo (Guest) on March 11, 2017

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Andrew Mchome (Guest) on November 26, 2016

Neema na amani iwe nawe.

Dorothy Majaliwa (Guest) on November 9, 2016

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Edward Lowassa (Guest) on June 29, 2016

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Alex Nyamweya (Guest) on June 25, 2016

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Michael Onyango (Guest) on March 25, 2016

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

David Chacha (Guest) on February 27, 2016

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Ruth Mtangi (Guest) on February 22, 2016

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Stephen Amollo (Guest) on January 22, 2016

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Grace Majaliwa (Guest) on October 29, 2015

Nakuombea 🙏

Monica Adhiambo (Guest) on September 5, 2015

Tumaini ni nanga ya roho

Charles Mchome (Guest) on August 23, 2015

Imani inaweza kusogeza milima

Charles Mrope (Guest) on July 28, 2015

Mwamini katika mpango wake.

Catherine Mkumbo (Guest) on May 16, 2015

Mungu akubariki!

Related Posts

Je, Kanisa Katoliki linakiri na kufundisha amri kumi za Mungu kama mwongozo wa maisha ya Kikristo?

Je, Kanisa Katoliki linakiri na kufundisha amri kumi za Mungu kama mwongozo wa maisha ya Kikristo?

Je, Kanisa Katoliki linakiri na kufundisha amri kumi za Mungu kama mwongozo wa maisha ya Kikristo... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu maisha ya watoto wachanga?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu maisha ya watoto wachanga?

Katika Kanisa Katoliki, watoto wachanga ni baraka kubwa kutoka kwa Mungu. Imani yetu inaamini kuw... Read More

Huruma ya Mungu: Ulinzi na Uongozi katika Maisha

Huruma ya Mungu: Ulinzi na Uongozi katika Maisha

Huruma ya Mungu: Ulinzi na Uongozi katika Maisha

Katika maisha yetu, tunaenda kupitia chan... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti ya Ndoa?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti ya Ndoa?

Karibu katika makala hii ambapo tutajifunza kuhusu imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti ya ... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu msamaha na rehema?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu msamaha na rehema?

Leo tutajadili kuhusu imani ya Kanisa Katoliki kuhusu msamaha na rehema. Kwa Wakatoliki, msamaha ... Read More

Heshima za Liturujia kwa Bikira Maria

Heshima za Liturujia kwa Bikira Maria

Read More
Ishi kama Penseli ili uwe mtu bora

Ishi kama Penseli ili uwe mtu bora

Muumbaji wa penseli alipomaliza kuiumba penseli yake aliiambia mambo muhimu ya kuzingatia ili iwe... Read More

Huruma ya Mungu: Chemchemi ya Upendo Usiokwisha

Huruma ya Mungu: Chemchemi ya Upendo Usiokwisha

Huruma ya Mungu: Chemchemi ya Upendo Usiokwisha

  1. Kama Mkristo Katoliki, tunajua k... Read More

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa haki na kulinda haki za binadamu?

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa haki na kulinda haki za binadamu?

Kanisa Katoliki ni moja kati ya makanisa makubwa duniani ambayo yamejikita katika kufundisha na k... Read More

Njia Bora ya Kuelewa Masomo ya Misa ya Dominika ya Jumapili

Njia Bora ya Kuelewa Masomo ya Misa ya Dominika ya Jumapili

Njia Bora ya Kuelewa Masomo ya Misa ya Dominika ya Jumapili

Moyo wangu unajaa furaha na sh... Read More

Njia Kuu 3 za Kuiishi Huruma ya Mungu

Njia Kuu 3 za Kuiishi Huruma ya Mungu

Read More
Kuishi katika Huruma ya Mungu: Njia ya Utakatifu na Ukarimu

Kuishi katika Huruma ya Mungu: Njia ya Utakatifu na Ukarimu

Kuishi katika Huruma ya Mungu: Njia ya Utakatifu na Ukarimu

  1. Kuishi katika huruma... Read More